ANGOLA YADAIWA KUPIGA MARUFUKU UISLAMU NA KUVUNJA MISIKITI





Angola imeripotiwa kuipiga marufu dini ya Kiislamu na kuanza kubomoa misikiti, na hivyo kuwa nchi ya kwanza ulimwenguni kuchukua hatua hiyo.

Siku ya Ijumaa, magazeti kadhaa katika nchi hiyo ya kusini mwa Afrika yalidaiwa kumnukuu Waziri wa Utamaduni wa nchi hiyo, Rosa Cruz e Silva, akisema kuwa “mchakato wa kuuhalalisha na kuuruhusu Uislamu haukuidhinishwa na Wizara ya Sheria na Haki za Binadamu... hivyo misikiti itafungwa mpaka taarifa zaidi itakapotolewa."

Silva alidaiwa kusema kuwa marufuku hiyo ni muhimu kwa kuwa Uislamu “unapingana na desturi za utamaduni wa Angola."

Baada ya hapo serikali ilianza programu ya ubomoaji wa misikiti na maeneo mengine ya Waislamu kama sehemu ya marufuku hiyo.

Uamuzi huo ni hatua mpya kabisa ya mlolongo wa jitihada za kupiga marufuku kile ambacho maafisa wa Angola wanakiita kuwa ni “madhehebu haramu ya dini.”

Hata hivyo, Mzizima 24 inaendelea kufuatilia kwa karibu ripoti za marufuku hiyo dhidi ya Uislamu, kwa maana hazijathibitishwa na vyanzo huru , kwa kuwa katiba ya Angola inatoa uhuru wa kuwa na dini kwa raia wote wa nchi hiyo.

Jana Jumatatu, afisa mmoja kwenye Ubalozi wa Angola mjini Washington D.C. alikanusha taarifa za nchi yake kuupiga marufuku Uislamu, akisema kuwa “Jamhuri ya Angola… ni nchi isiyoingilia masuala ya dini.”

“Tuna dini nyingi kule. Kuna uhuru wa dini. Kuna Wakatoliki, Waprostanti,  Wa-Baptist, Waislamu na hata Walokole,” alisema afisa huyo.

Mwezi Oktoba, Waislamu wanaoishi manispaa ya Viana Zango mjini Luanda, walipigwa na butwaa baada ya kukuta mnara wa msikiti wao ukiwa umevunjwa vipande vipande. Mamlaka za serikali hazikutoa maelezo yenye kujitosheleza kuhusu hatua hiyo.


Idadi ya raia wa nchi hiyo yenye wakazi milioni 19, ni Wakristo. Kuna Waislamu wanaokadiriwa kuwa 80,000 mpaka 90,000, na idadi yao inaongezeka.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment