UTURUKI KUZINDUA TREINI YA CHINI YA BAHARI


Turkey ready to take first ride on landmark undersea train line


Leo Oktoba 29 Uturuki inaandika historia katika sekta ya maendeleo, hasa miundombinu kwa kuzindua mradi mkubwa wa usafiri, unaojulikana kama  Marmaray. Mradi huu utakuwa kiunganishi cha pande mbili za mji wa Istanbul, uke wa Ulaya na wa Asia kupitia treini ya abiria ya chini ya bahari.

Itakumbukwa kuwa mji wa Istanbul ndio mji pekee duniani unaopatikana kwenye mabara mawili, Asia na Ulaya kwa pande hizo mbili kutengenishwa na mkondo maarufu wa Phosphorous.

Mradi huu unaozinduliwa leo ni utekelezaji wa ndoto ya kiongozi mmoja wa dola ya Kiuthmaniya miaka 153 iliyopita.

Mradi huu utakaozinduliwa na Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Recep Teyyip Erdogan, unalenga kuondoa tatizo la msongamano barabarani katika mji huo na kupunguza muda wa kusafiri baina ya pande hizo mbili za mji. Marmaray, ambayo ndio njia ya kwanza ya chini ya bahari duniani kuyaunganisha mabara mawili, itabeba abiria 75,000 kwa saa na karibu wasafiri milioni 1 kwa siku.





Marmaray itakuwa kiunganishi baina ya mabara hayo kwa njia ya chini ya bahari itakayopita jirani kabisa na Mkondo wa Bosporus unaoziunganisha Bahari Nyeusi (Black Sea) na Bahari ya Marmara na kuelekea kwenye Bahari ya Meditterania.

Njia ya Marmaray itakuwa na stesheni  tatu za chini ya ardhi katika manispaa za Yenikapı, Sirkeci na Üsküdar na vituo 36 juu ya ardhi.

Ni muhimu kuashiria hapa kuwa mpaka mwaka 2020 Uturuki inapanga kuwa kati ya nchi 10 tajiri duniani.


Aidha, Uturuki inafanya maendeleo makubwa sana katika sekta mbalimbali ikiwa haina maliasili kama madini, mbunga za wanyama, misitu, mafuta, gesi na kadhalika. Bali rasilimali watu ndiyo imewafikisha huko na uzalendo wa wananchi wake.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment