RIPOTI: SIMU YA KANSELA ANGELA MERKEL ILIRIKODIWA NA WAMAREKANI KWA MIAKA KUMI

 



Wakati suala la ujasusi unaofanywa na Marekani kwa mawasiliano ya viongozi na mamilioni ya watu wengine duniani kote likiwa linaitikisa Jumuiya ya Umoja wa Ulaya, ripoti mpya iliyochapishwa hivi karibuni imeonesha kuwa Marekani imekuwa ikiyamulika mawasiliano ya simu ya Kansela wa Ujerumani, Angela Markel tangu mwaka 2002.

Gazeti la kila wiki la nchini Ujerumani, Der Spiegel, limesema katika ripoti iliyochapishwa jana kuwa liliona nyaraka za siri kutoka Shirika la Usalama la Marekani (NSA) zinazoonesha kuwa simu ya mkononi ya Merkel iliwekwa katika orodha maalumu inayofuatiliwa na Shirika hilo tangu mwaka 2002.

Ripoti hiyo imeongeza kuwa mwezi Juni 2013 namba ya simu ya mkononi ya kansela huyo wa Ujerumani bado ilikuwa katika orodha ya simu zinazopekuliwa na shirika hilo.

Maepna Ijumaa, serikali ya Ujerumani ilisema kuwa wakuu wake wa usalama wangetembelea Washington mapema ili kuchunguza sakata hilo.

Msemaji wa serikali hiyo, Georg Streiter, amesema kuwa wakuu wa ujasusi wa ndani na nje watakutana na maafisa mbalimbali kutoka Ikulu ya Marekani na wale wa NSA.

Wakati huo huo, msemaji wa Shirika la Usalama la Marekani, Caitlin Hayden alisema kuwa Wajerumani hao watakaribishwa, lakini hakueleza kwa undani zaidi ni kwa jinsi gani Washington itashughulikia ghadhabu iliyooneshwa na Wajerumani dhidi ya vitendo vya kurikodi mazungumzo ya viongozi wake.

Siku ya Alhamisi, gazeti la The Guardian liliripoti kuwa NSA ilirikodi mazungumzo ya simu za viongozi 35 wa mataifa mbalimbali.

Snowden, mfanyakazi wa zamani wa CIA, alivujisha programu kubwa mbili za siri mno kutoka serikali ya Marekani zinazotekelezwa na NSA na FBI, ambapo huzifanyia ujasusi na kurikodi mamilioni ya simu za wananchi wa Marekani na wale wa Ulaya na kutega taarifa za mawasiliano ya intaneti kutoka kwenye makampuni makubwa ya mitandao kama vile Facebook, Yahoo, Google, Apple, na Microsoft.


Sakata la NSA lilifumuka zaidi baada ya Snowden kufichua taarifa za Marekani kuzifanyia ujasusi nchi rafiki.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment