WABAKAJI WAHUKUMIWA KIFO




Jaji wa mahakama moja katika mji wa New Delhi nchini India ametoa hukumu ya adhabu ya kifo kwa wanaume wanne waliokutwa na hatia ya kumbaka mwanafunzi wa kike mwenye umri wa miaka 23 kwenye basi mwaka jana.

Watu hao walikutwa na hatia ya kumbaka binti huyo mwezi Desemba 2012  kwenye gari iliyokuwa ikitembea katika mji mkuu wa nchi hiyo na kumjeruhi vibaya sana, hali iliyompelekea kufariki dunia wiki mbili baadaye.

Mshitakiwa mwenye umri mdogo zaidi, ambaye alishitakiwa katika kesi hiyo, ameshahukumiwa adhabu ya kifungo cha miaka mitatu na kuwekwa katika jela maalumu ya watoto, huku mshitakiwa wa tano akijinyonga gerezani mwezi Machi.

Binti huyo amekuwa alama ya hatari zinazowakabili wanawake nchini India ambapo tukio moja la ubakaji huripotiwa kila baada ya dakika 21.

Unyama huo uliamsha moto wa hasira na maandamano yaliyoitikisa nchi nzima na kuilazimisha serikali kuweka sheria maalumu juu ya usalama wa wanawake.

Katika miaka ya hivi karibuni, India imekuwa na mwenendo tofauti kuhusu adhabu ya kifo.

Mahakama za India hutoa adhabu za vifo zipatazo 130 kila mwaka, lakini ni watu watatu pekee ndio walionyongwa ndani ya miaka 17.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment