UFARANSA YAMWACHIA HURU MSHUKIWA WA MAUAJI YA KIMBARI YA NCHINI RWANDA

 Rwandan soldiers watch the skulls of victims of the 1994 genocide. (file photo)


MAHAKAMA moja nchini Ufaransa imeamuru kuachiliwa huru kwa aliyewahi kuwa kanali wa jeshi anayetafutwa na Rwanda kuhusiana na mauaji ya kimbari yaliyoikumba nchi hiyo mwaka 1994.

Mahakama hiyo iliyopo katika mji wa Douai, kasikazini mwa Ufarsana, jana iliagiza kuachiwa huru kwa Laurent Serubuga na kulitupilia mbali ombi lililotolewa na Rwanda la kutaka mshukiwa huyo apelekwe kujibu mashitaka nchini Rwanda.

Mahakama hiyo ilisema kuwa kanali huyo wa zamani hawezi kushitakiwa kwa uhalifu huo kwa kuwa haukuingizwa katika sheria ya uhalifu ya Rwanda wakati vurugu hizo zikitokea.


Aidha, mahakama hiyo iliyatupilia mbali mashitaka yaliyotolewa dhidi ya Serubuga, ikisema kuwa kibali cha kukamatwa kilitolewa zaidi ya miaka 10 baada ya mauaji hayo ya kimbari.


naye Mkuu wa Muungano wa Jumuiya za Kiraia nchini Rwanda, Alain Gautier, alielezea kusikitishwa kwake, akisema kuwa Serubuga alikuwa “mtu muhimu katika mauaji ya kimbari.”

“Ni uamuzi wa kusikitisha sana. ni mara ya 15 au 16 Ufaransa ikikataa kuwarudisha Rwanda washukiwa wa mauaji,” alisema.

Serubuga alikamatwa mwezi Julai katika mji wa Cambrai ulio kaskazini mwa Ufaransa kwa hati ya kimataifa iliyotolewa na Rwanda.

Serubaga mwenye umri wa miaka 75, aliwahi kuwa naibu mkuu wa majeshi wa Rwanda wakati wa mauaji ya Kimbari ya 1994, ambapo kabila la Wahutu liliwahua watu wapatao 800,000, wengi wao wakiwa Watutsi.

Mauaji hayo yalitokea baada ya ndege iliyokuwa imembeba Rais wa Rwanda wa wakati huo, Juvenal Habyarimana, kuripuliwa mnamo Aprili 6, 1994. Mauaji hayo yalidumu kwa siku 100 na hivyo kujulikana kama “Siku 100 za Jahanamu.”



Mwaka 2011, Kanali Theoneste Bagosora, alielezewa na mahakama ya kimataifa kuhusu Rwanda kama mpangaji wa mauaji ya kimbari na kuhukumiwa adhabu ya miaka 35 jela.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment