UNHCR YAISHUTUMU TANZANIA

 

WAKATI serikali ya Tanzania ikiendelea na operesheni ya kuwarejesha makwao wahamiaji haramu, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), limedai kuwa raia hao wamenyanyaswa.

Kwa mujibu wa taarifa ya shirika hilo iliyochapishwa na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), takriban wakimbizi 25,000 kutoka Burundi wameondoshwa Tanzania kwa nguvu katika mwezi mmoja uliopita.

Afisa wa shirika hilo, alisema kuwa malori yanayowasafirisha Warundi hao yamekuwa yakivuka mpaka kila siku, huku wengi wao wakikosa maji na chakula.

Kwa sasa Tanzania iko kwenye operesheni ya kuwafukuza wahamiaji waliojipenyeza nchini bila kufuata utaratibu wa kupata vibali halali.

Mpaka sasa raia wengi wa mataifa mbalimbali wamekamatwa na kurudishwa makwao huku nchini za Burundi, Rwanda na Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Kongo zikiongoza kwa idadi ya watu.

Kwa miaka mingi Tanzania iliwahifadhi mamilioni ya wakimbizi waliokuwa wakiyakimbia mapigano katika nchi jirani.

Takriban watu milioni moja walitoroka kutoka Burundi na kuingia Tanzania wakati wa mgogoro wa wenyewe kwa wenyewe wakati vita vilipozuka mwaka 1993.


Wengi walirejea kwa hiari wakati amani ilipopatikana mwaka 2006.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment