UMOJA WA MATAIFA: SILAHA ZA KEMIKALI ZILITUMIKA SYRIA

 



WAKAGUZI wa Umoja wa Mataifa wamethibitisha kutumika kwa silaha za kemikali katika shambulizi moja lililofanyika mwezi uliopita karibu na mji mkuu wa Syria, Damascus, lakini haikuunyooshea kidole upande wowote.


Kwa mujibu wa ripoti hiyo iliyotolewa leo na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon, sampuli za kemikali zilizochukuliwa zinaonesha kuwa makombora ya ardhini yenye sumu ya sarin yalitumika katika eneo la Ghouta Agosti 21.

"Tunahitimisha kwamba silaha za kemikali zimetumika katika mgogoro unaoendelea baina ya pande mbalimbali katika Jamhuri ya Kiarabu ya Syria…dhidi ya raia, wakiwemo watoto, kwa kiwango kikubwa,” inasema ripoti hiyo.

Mamia ya watu waliuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa katika shambulizi moja la kemikali katika viunga vya Damascus vya Ain Tarma, Zamalka na Jubar mnamo Agosti 21.


Makundi ya upinzani nchini humo yalidai kuwa shambulizi hilo lilifanywa na jeshi la utawala wa Damascus.

Hata hivyo, serikali imekuwa ikikanusha vikali madai hayo na kusema kuwa shambulizi hilo lilifanywa na makundi ya waasi ili kuchochea ghadhabu ya jumuiya ya Kimataifa dhidi ya serikali hiyo na ili kuweka shinikizo la uingiliaji kijeshi kutoka nje.


Kufuatia shembulizi hilo, Marekani ilitaka kuchukuliwa kwa hatua ya kijeshi dhidi ya Damascus. Serikali ya Syria iliepusha hujuma hiyo ya kijeshi kwa kuukubali mpango wa Urusi wa kuyaweka maghala yake ya silaha za kimataifa chini ya uangalizi wa kimataifa na kisha ziharibiwe.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment