NDEGE ZA UTURUKI ZAITUNGUA HELIKOPTA YA SYRIA

Turkish warplanes shoot down Syrian helicopter
Helikopta ya jeshi la Syria ikiwa katika uwanja wa jeshi wa Minnigh baada ya kutunguliwa







NAIBU Waziri Mkuu wa Uturuki Bulent Arinc amewaambia waandishi wa habari kuwa ndege za kivita za Uturuki zimeidondosha helikopta ya jeshi la Syria baada ya kuingia katika anga yake.

Helikopta hiyo aina ya MI-17 mali ya Syria ilidondosha katika jimbo la kusini la Hatay baada ya kupenya umbali wa kilometa 2 katika anga ya Uturuki.

Arinc alisema huwa hapakuwa na taarifa kuhusu kilichowakuta marubani wa helikopta hiyo kwa sababu ilienda kuangukia katika ardhi ya Syria. Vilevile alieleza kuwa jeshi la anga la Uturuki liliionya helikopta hiyo mara kadhaa kuondoka katika anga yake kabla ya kupigwa kwa makombora.

Ripoti ambazo hazijathibitishwa rasmi zinasema kuwa wapiganaji wanaopigana dhidi ya serikali ya Syria wamewaua marubani hao. Pia kuna ripoti zinazosema kuwa rubani mmoja alikamatwa na waasi huku mwingine akiwa hajulikani aliko.

Mpaka sasa serikali ya Syria haijatoa maelezo yoyote juu ya tukio hilo.


Tukio hilo linakuja mwaka mmoja baada ya jeshi la anga la Syria kuidondosha ndege ya kivita ya Uturuki baada ya kuingia katika anga yake. Inasemekana kuwa ndege hiyo ilidondokea upande wa Syria jirani na kijiji cha Um al-Touyour. Hata hivyo, Uturuki ilisisitiza kuwa ndege yake iliingia katika anga ya Syria lakini ikaondoka haraka baada ya kuonywa, na ilitunguliwa ikiwa katika anga ya kimataifa dakika kadhaa baadaye.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment