RIPOTI: MWANAUME MMOJA KATI YA WANAUME WANNE WA ASIA HUFANYA UBAKAJI





Takribani robo ya wanaume sita kutoka nchi za Asia waliohojiwa katika utafiti uliofanywa na Umoja wa Mataifa wamekiri kufanya ubakaji angalau mara moja.

Utafiti huo uliochapishwa Jumanne iliyopita katika Jarida la  Lancet Global Health uliwahoji zaidi ya wanaume 10,000 katika maeneo mbalimbali ya nchi za  Bangladesh, China, Cambodia, Indonesia, Sri Lanka, na Papua New Guinea.

Karibu asilimia 10 ya waliohojiwa walisema kuwa walifanya mapenzi ya kulazimisha na mwanamke ambaye sio mshirika wao. Lakini asilimia hiyo ilipanda mpaka kufikia 24 pindi washirika wao walipojumuishwa katika swali.

Takriban nusu ya wale waliokiri walieleza kuwa waliwahi kuwabaka wanawake mbalimbali. Wengi walisema kuwa hawakukumbana na mkono wa sheria kwa vitendo vyao hivyo.

Wachunguzi walionya kuwa uchunguzi wao hauakisi takwimu rasmi za vitendo vya ubakaji katika nchi husika, kwa sababu ulifanyika katika maeneo tisa tu. Hata hivyo, utafiti huo utasaidia kuhamasisha juhudi za kuzuia vitendo vya ubakaji na dhulma dhidi ya wanawake.

Utafiti ulibaini kuwa sababu za dhulma hizo dhidi ya wanawake zinatofautiana kutoka eneo moja kwenda jingine. Dhulma shidi ya watoto, matumizi ya ulevi, umasikini, migogoro na vita katika maeneo husika ni miongoni mwa sababu za vitendo hivyo.


Karibu robo tatu ya wale waliokiri kubaka walisema kuwa walifanya hivyo kukidhi matamanio ya kimwili. Asilimia 60 walisema kuwa walibaka kwa ajili ya burudani, huku asilimia 40 wakisema kuwa walibaka ili kumuadhibu mwanamke husika.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment