SASA ALSHABAAB WATISHIA KUWAUA MATEKA WOTE WANAOWASHIKILIA




WAPIGANAJI wa kundi la Al-Shabaab la Somalia, wameionya serikali ya Kenya isitumie nguvu kuingia katika jengo la Westgate, kwa kuwa matokeo yatakuwa mabaya.





Kwa mujibu wa taarifa ya sauti iliyotolewa na kundi hilo, Al-Shabaab wameonya kwamba watawaua mateka wote wanaowashikilia katika jengo hilo iwapo Jeshi la Ulinzi la Kenya (KDF) na mashirika mengine ya usalama watajaribu kutumia nguvu kuingia kwenye jengo hilo.

“Askari wa Israeli na Kenya vimejaribu kuingia ndani kwa nguvu lakini hawakuweza, Mujahideen (wapiganaji) watawaua mateka wote iwapo maadui watatumia nguvu”, alisema msemaji wa Al-shabaab, Sheikh Ali Mahmud Rage (pichani).

Hata hivyo, vikosi vya usalama vimeapa kuendelea na zoezi la uokozi na watafanya kila linalowezekana hilo lisitokee.


Mpaka sasa watu 69 wameshauawa na wengine wapatao 200 wamejeruhiwa.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment