RAIS WA ZAMBIA ATISHIA KULIVUNJA BUNGE

Zambian President Michael Sata
Rais wa Zambia Michael Sata



RAIS wa Zambia, Michael Sata ametishia kulivunja bunge la nchi hiyo akiwatuhumu mawaziri kushindwa kuitetea serikali dhidi ya mashambulizi ya upinzani.

Habari hiyo imekuja baada ya utawala wa Sata ambao upo madarakani kwa miaka miwili sasa kushutumiwa kwa kuwa na mawaziri wengi.

"Kwa nini hamzungumzi? Kwa nini mnakaa kimya?” aliuliza Sata katika kikao chake na baraza la mawaziri leo.

"Kama hamuwezi kuwa mnavyotakiwa kuwa niambieni ili nilivunje bunge na kuitisha uchaguzi mkuu.”


Vyama vya upunzani nchini humo vimelikosoa vikali baraza hilo, wakimtuhumu Sata kuwa na mawaziri wengi, ambao ni maswahiba wa rais.

Kwa mujibu wa katiba ya Zambia, uchaguzi mpya unapaswa kufanyika ndani ya siku 9 iwapo bunge litavunjwa.

Sata aliwataka mawaziri kujibu shutuma kutoka vyama vya upinzani, hususan kutoka kwa kiongozi wa chama cha United Party for National Development (UPND), Hakainde Hichilema.

"Tunachafuliwa kushoto, kulia na katikati. Leo Hichilema anasema baraza hili la mawaziri limevimbiwa, siku nyingine akasema baraza hili ni la ukoo na nyinyi mnakaa kimya bila kumjibu… mnadhani nani atakayewajibia?” alisema Sata.


Uchaguzi mkuu wa Zambia umepangwa kufanyika mwaka 2016.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment