MABINTI WA KITUNISIA WATUMIKA KWA HUDUMA ZA NGONO NCHINI SYRIA







WAZIRI wa mambo ya ndani wa Tunisia amesema kuwa idadi kadhaa ya mabinti wa Kitunisia wamekuwa wakisafiri kwenda nchini Syria na kutumika katika shughuli za ngono kwa ajili ya makundi yanayopigana dhidi ya serikali ya nchi hiyo.

Jana alihamisi, Waziri huyo, Lotfi Ben Jeddou aliwaambia wabunge kuwa wanawake wa Kitunisia waliosafiri kwenda Syria wamerejea na ujauzito kutokana na kugeuzwa kuwa washirika wa ngono kwa mamia ya wapiganaji wa makundi hayo, kwa kile kinachoelezwa kuwa ni “jihadi ya ndoa.”

Bin Jeddo alisema kuwa wizara ya mambo ya ndani imewapiga marufuku wanawake 6,000 wasisafiri kwenda Syria tangu Machi 2013 na kuwatia nguvuni watuhumiwa 86 wanaotengeneza “mitandao” inayotumika kuwasafirisha vijana wa Kitunisia kwenda kushiriki vita nchini humo.

“Walikuwa na mahusiano ya kijinsia na waasi 20, 30, 100. Baada ya kutumika kwa kazi hiyo waliyoiita 'jihad al-nikah' - (jihad ya ndoa) – wanarudi nyumbani wakiwa wajawazito,” alisema Ben Jeddou.

Waziri huyo hakusema ni wanawake wangapi walioenda Syria, lakini ripoti za vyombo vya habari nchini humo vinaeleza kuwa ni mamia ya wanawake.

Aidha, waziri huyo aliyakosoa vikali makundi ya haki za kibinaadamu yanayoukosoa uamuzi wa serikali kuwapiga marufuku wale wanaosafiri kwenda Syria kupigana vita. Vijana wengi waliokumbwa na marufuku hiyo ni wale walio chini ya umri wa miaka 35.


“Vijana wetu wanawekwa msitari wa mbele wa mapambano na wanafundsihwa jinsi ya kuiba na kuvamia vijiji,” alisema Bin Jeddo.


Naye Mufti wa zamani wa Tunisia, Sheikh Othman Battikh, mnamo tarehe 13 Aprili alisema kuwa mabinti wa Kitunisia walikuwa “wakihadaiwa”  kwenda Syria kutoa huduma za ngono kwa waasi wanaopambana kuundoa utawala wa Rais Bashar al-Assad.

Mufti huyo, ambaye baadaye aliondolewa kwenye wadhifa wake, aliielezea hiyo inayoitwa “jihadi ya ngono” kuwa ni aina ya ukahaba.

“Sasa hivi wanawasukuma mabinti kwenda Syria kwa ajili ya Jihad. Mabinti wadogo 13 wamepelekwa kwa ajili ya huduma ya ngono. Hiki ni kitu gani? Huu ni ukahaba. Ni uharibifu wa kimaadili,” alisema mufti huyo wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Mwezi Agosti mwaka huu, mkurugenzi mkuu wa usalama wa umma, Mustafa Bin Omar alisema kuwa “jihadi ya ngono” ilikuwa imeshamiri sana magharibi mwa nchi hiyo ambapo makundi ya wapiganaji wamejichimbia.

Bin Omar aliwaambia waandishi wa habari kuwa makundi ya wanamnagambo wanawatumia mabinti wadogo, waliojifunika nyusoni, kutoa huduma za kijinsia kwa wapiganaji wa kiume.


CHANZO: al-Arabiya/ Mitandao ya kijamii
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment