PAKISTAN YAMWACHIA HURU KIONGOZI MWANDAMIZI WA TALEBAN






AFISA mwandamizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Pakistan amesema kuwa nchi hiyo imemuachia huru kiongozi mwandamizi wa Taliban la Afghanistan, Abdul Ghani Baradar.


Baradar, ambaye alielezwa kuwa kiongozi namba mbili wa wapiganaji wa Taleban ameachiwa huru leo Jumamosi.

“Ndiyo, Baradar ameachiwa huru,” msemaji wa wizara ya mambo ya ndani,  Omar Hamid, alisema bila kutoa taarifa zaidi kuhusu mazingira ya kuachiwa kwa mfungwa huyo.

Mapema Ijumaa, Wizara ya Mambo ya Nje ya Pakistan ilisema kuwa kuachiwa huru kwa Baradar mwenye umri wa miaka 45, anayejulikana pia kama Mullah Baradar, kungesaidia mchakato wa amani nchini Afghanistan.

“Ili kuweka mazingira mazuri ya mchakato wa maridhiano nchini Afghanistan, kiongozi huyo wa Taliban, Mullah Abdul Ghani Baradar, angeachiwa kesho (leo),” ilisema taarifa ya wizara hiyo.

Serikali ya Afghanistan imekuwa ikiitolea wito Pakistan kumuachia huru Baradar, ambaye alitiwa nguvuni katika mji wa Karachi Julai 2010.

Rais wa Afghanistan, Hamid Karzai, anafanya juhudi za kuanzisha mazungumzo ya moja kwa moja baina ya serikali yake na wapiganaji wa Taliban ili kurejesha amani iliyozorota nchini mwake.

Tangu mwaka jana, Pakistan imewaachia huru wafungwa wapatao 33 wa Kitaliban baada ya kuombwa na Afghanistan ili kusukuma mbele juhudi za mazungumzo ya amani.

Kwa upande wa serikali ya Afghanistan iliupokea kwa furaha uamuzi huo. “Tunaikaribisha na kuipokea hatua hii iliyochukuliwa. Tunaamini kuwa hili litasaidia kwenye mchakato wa amani ya Afghanistan,” alisema msemaji wa Rais Karzai, Aimal Faizi.

Marekani na waitifaki wake waliingia vitani nchini Afghanistan Oktoba mwaka 2001 katika kile kilichoitwa kuwa ni vita dhidi ya ugaidi.


Hatua hiyo iliwaondoa Taliban madarakani, lakini baada ya zaidi ya miaka 11, vikosi hivyo vya kigeni havijaweza kuleta usalama nchini humo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment