LIGI KUU TANZANIA: SIMBA YAUA 6-0, YANGA SC, AZAM FC ZABANWA





MABAO 6-0 iliyoyapata Simba Sc leo dhidi ya Mgambo Shooting, yameiwezesha timu hiyo kufikisha poiunti 10 na hivyo kukalia usukani wa ligi hiyo.

Aidha,mabingwa watetezi wa ligi hiyo Yanga Sc, wameendelea kubanwa tena mjini Mbeya baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Tanzania Prisons katika mchezo uliopigwa kwenye dimba la Sokoine mjini humo.Ikumbukukwe kuwa Yanga ilitoka sare ya bao 1-1 jumamosi iliyopita dhidi ya Mbeya City katika mchezo uliopigwa kwenye uwanja huo.

Mshambuliaji wa Kimataifa wa Simba Amis Tambwe ambaye pia ni kinara wa mabao katika ligi hiyo kwa sasa, aliiandikia mabao manne huku Haruna Chanongo akifunga mawili.

Aidha, Wanalambalamba Azam Fc nao wamebanwa mbavu na vibonde wa ligi hiyo Ashanti United baada ya kulazimisha sare ya bao 1-1 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Azam Complex, Chamazi jijini Dar es Salaam.

Matokeo mengine ya ligi hiyo ni kama ifuatavyo:

Jkt Ruvu V Ruvu Shooting      0-1
Mtibwa Sugar V Mbeya City   0-0
Rhino V Coastal Union             1-1

Kagera Sugar V Jkt Oljoro     2-1
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment