KASISI WA KIMAREKANI AFUNGWA MIAKA 50 JELA KWA KUTENGENEZA PICHA ZA UCHI ZA WATOTO

 




KASISI mmoja wa Kanisa Katoliki katika jimbo la Missouri nchini Marekani amehukumiwa adhabu ya kifungo cha miaka 5 jela kwa kutengeneza picha na filamu za uchi za watoto.

Adhabu hiyo ilitolewa na Jaji Gary Fenner, ambapo kasisi Shawn Ratigan, mwenye umri wa miaka 47, atatumikia kipindi kilichobaki cha maisha yake katika jela kwa sababu katika mfumo wa jela za Marekani hakuna msamaha wa kutoka jela ya kumaliza kifungo ambao hutolewa kwa watu kwa sharti la kutotenda kosa.

Mwezi Agosti mwaka jana, Ratigan alikiri kosa katika mashitaka matano ya kuzalisha au kujaribu kuzalisha filamu za uchi za watoto.

Kwa mujibu wa waendesha mashitaka, aliwapiga picha watoto wa kike ndani na jirani na makanisa aliyokuwa akifanya kazi katika Mji wa Kansas, Missouri.

Mwezi desemba 2010, fundi mmoja wa kompyuta alikuta maelfu ya picha za watoto wadogo watano katika kompyuta ndogo (laptop) ya Ratigan wakati akifanya kazi kwenye kompyuta hiyo.

Fundi hiyo alichukua uamuzi wa kuripoti kisa hicho kwa maafisa wa Kanisa Katoliki la Mt. Joseph katika Dayosisi ya Mji wa Kansas. Hata hivyo, Askofu Robert Finn wa Dayosisi hiyo hakuzikabidhi polisi picha hizo na aliamua kumpeleka Ratigan kufanyiwa uchunguzi wa akili.

Matukio hayo yalisababisha Askofu Finn ashitakiwe kwa makosa ya jinai na kumfanya kuwa afisa wa ngazi ya juu wa Kanisa Katoliki nchini Marekani kushhitakiwa kwa makosa ya uhalifu na jinai.

Ratigan, aliwaomba msamaha waathirika na familia zao kabla ya kuhukumiwa. Hata hivyo, alisema kuwa hakutakiwa kupewa adhabu ya kifungo cha miaka 50 jela.


“Jela ni jehanamu. Ninajua ninastahiki adhabu ya miaka 15, lakini miaka 50? Sidhani,” alisema Ratigan.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment