KANSELA ANGELA MARKEL KUSHINDA KWA KISHINDO UCHAGUZI MKUU







KURA za maoni zinaonesha kuwa chama cha Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel, kinatarajiwa kupata ushidni mkubwa katika viti vya bunge katika uchaguzi mkuu wa nchi hiyo.

Tathmini zilizofanywa na vituo vya televisheni leo kuhusu maoni ya wananchi zilionesha kuwa Chama cha Markel cha Christian Democratic Union (CDU) kitashinda viti 304 kati ya 606 katika bunge.

Hiyo ina maana kwamba muungano wake wa wahafidhina hautahitaji washirika wengine na wanaweza kuunda serikali peke yao.

Kura za maoni za mapema zilionesha kuwa chama cha Markel kilihitaji kuunda kile kinachoitwa muungano mkubwa na upinzani wa mrengo wa kushoto wa Chama cha Social Democratic.

Haya yanakuja wakati Chama cha upinzani cha Alternative fur Deutschland (AfD) kikiwa hakina uhakika wa kuingia bungeni. Maoni ya sasa yanaonesha kuwa chama hicho hakiwezi kupata asilimia tano ya viti vyote.


Akipewa nuvu na matokeo haya, Merkel ameahidi kufanya makubwa zaidi katika miaka mingine minne ya uongozi wake.  

“Kwa pamoja tutafanya kila kitu katika miaka mingine minne ili kuifanya kuwa yenye mafanikio kwa Ujerumani,” alisema Markel.

Wakati wa kampeni mjini Berlin jana, Merkel aliuambia umati wa wafuasi wa chama cha Christian Democrat kuanza kukusanya nguvu tena kutoka kwa raia wa Ujerumani.

“Mimi binafsi ninawaomba wananchi wa Ujerumani: nipeni nguvu zaidi ili niweze kuitumikia Ujerumani kwa miaka mingine minne,” alisema Markel.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment