CHAMA CHA ‘MUSLIM BROTHERHOOD’ CHAPIGWA MARUFUKU NCHINI MISRI







MAHAKAMA mjini Cairo imezifungia na kuzipiga marufuku shughuli zote za vuguvugu la Udugu wa Kiislamu kama taasisi isiyokuwa ya Kiserikali, kwa mujibu wa duru za kimahakama.

Hukumu ya mahakama hiyo inajumuisha kuzishikilia mali, rasilimali na makao makuu ya vuguvugu hilo.

"Mahakama inapiga marufuku shughuli za vuguvugu la Udugu wa Kiislamu na taasisi yake isiyokuwa ya Kiserikali na shunguli zote inazoshiriki na taasisi yoyote inayotokana nacho,” vyombo vya habari vilimnukuu jaji Mohammed al-Sayed akisoma hukumu hiyo.

Mahakama imelipa baraza la mawaziri pendekezo la kuunda kamati huru kufuatilia utekelezaji wa hukumu hiyo.

Wengi wanaamini kuwa hukumu hiyo inaandaa uwanja kwa jeshi kuwatia nguvuni waandamanaji wanaliunga mkono vuguvugu hilo.

Jumuiya ya Udugu wa Kiislamu ilianzishwa mapema mwaka huu kama Taasisi isiyokuwa ya Kiserikali (NGO). Kiongozi wa zamani wa vuguvugu hilo,  Mohammed Mahdi Akef, ndiye aliyekuwa mwenyekiti wake. Viongozi wa jumuiya hiyo si wote wanaotoka katika vuguvugu hilo au Chama chake cha Uhuru na Uadilifu.


Chama cha Uhuru na Uadilifu ambacho ni tawi la kisiasa la vuguvugu hilo kilishinda uchaguzi wa bunge na urais baada ya kiongozi wa zamani wa taifa hilo, Husni Mubarak, kung’olewa katika mapinduzi ya wananchi ya mwaka 2011.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment