AL-SHABAAB WATETEA SHAMBULIZI LA NAIROBI






Al Jazeera: Ni zaidi ya miaka miwili sasa tangu askari wa Kenya walipoingia Somalia kupambana na al-Shabaab. Kwa nini Al-Shabaab waishambulie Nairobi leo na sio kabla?

SHEIKH ABULAZIZ ABU MUSCAB: Tumechelewa kuishambulia Nairobi. Hatufanya hivyo mapema kwa sababu walikuwa wakitarajia kuwa tutashambulia. Lengo letu ni kumshambulia adui anapokuwa hana matarajio ya kushambuliwa. Mara hii hawakutarajia kuwa tutawashambulia. Tulichagua muda mzuri wa kushambulia.

AJ: Hii ni mara ya kwanza kwa Al-Shabab kuishambulia Nairobi?

SA: Hilo sio muhimu. La muhimu ni kwamba sisi ndio tulioshambulia. Sio muhimu kusema kama tuliwahi kushambulia huko nyuma au la.

AJ: Shambulizi hili limefanyika kwenye kituo cha Biashara cha Westgate, ambapo wakati linashambuliwa lilikuwa limejaa watu. Kwa nini Al-Shabaab inashambulia eneo lililojaa raia?

SA: Sehemu tuliyoshambulia ni kituo cha biashara cha Westgate. Ni mahali ambapo watalii kutoka duniani kote huja kununua vitu, ni mhali ambapo wanadiplomasia hukutana. Ni mahali ambapo viongozi wa Kenya huenda kupumzika na kubarizi. Westgate ni mahali ambapo kuna maduka ya Wayahudi na Wamarekani. Hivyo, tumewashambulia.

Kuhusu vifo vya raia, Kenya ndiyo inayotakiwa kuulizwa kwanza kwa nini waliwaua raia wa Kisomali katika makambi ya wakimbizi? Kwa nini waliua watu wasiokuwa na hatia katika mikoa ya Gedo na Jubba. Wao ndio wanaotakiwa kuulizwa kwanza kabla yetu.

AJ: Al-Shabab inadai kuwa inawatetea Waislamu na hususan Wasomali. Baadhi ya watu waliouawa na kujeruhiwa katika tukio hili wanaona kuwa hili ni kinyume na madai yenu.

SA: Historia inatuunga mkono katika madai yetu. Sisi ndio pekee tunaowatetea Wasomali na Somalia. Sisi ndio kundi pekee linalopigana na maadui wa muda mrefu wa Somalia. Sisi ndio pekee tunaoweza kuwaambia maadui wa Somalia “hapana”.

Kuhusu kupotea kwa uhai wa watu, kuna askari wa Kenya wanaofyatulia risasi wapiganaji wetu. Kuna majibishano ya risasi. Hakuna ushahidi kwamba risasi zetu ndizo zilizowaua.

Tuliwaachia huru Waislamu wote tulipolidhibiti jengo. Mashuhuda wametuunga mkono juu ya hili.

AJ: Unadhani shambulizi hili litaifanya Kenya iyaondoshe majeshi yake kutoka Somalia?

SA: sisi sio tunaotakiwa kujibu hili swali. Serikali ya Kenya ndiyo inayotakiwa kujibu.  Uamuzi wa kuwaondoa au kutowaondoa askari ni wa kwao. Wasipoondoka, mashambulizi kama haya yatakuwa ya kawaida nchini Kenya. Iwapo hawataondoka mashambulizi kama haya yataendelea kutokea katika miji ya Kenya kila siku.

AJ: Kabla ya majeshi ya Kenya kuingia Somalia Oktoba 2011, uhusiano wa Al-Shabaab na serikali ya Kenya ulikuwa vipi?

SA: Siku zote tulijua kwamba Kenya ni adui wa watu wa Somalia. Tulilijua hili tulipoidhibiti mikoa ya mpakani. Tulitarajia kuwa watatuvamia. Hatuwaamini na wao hawatuamini.

AJ: Kenya inasema kuwa itawasaka  wahalifu waliotekeleza shambulizi hili na hawatakaa mpaka wawashinde. Unasemaje kuhusu hili?

SA: Sisi sio wahalifu. Sisi tunachokifanya ni kujilinda na kulinda haki zetu, haki za Wasomalia.

Leo hii hakuna mwenye rikodi mbaya ya uhalifu kama Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta. Anazungumzia makumi ya watu waliouawa katika jengo la Westgate ilhali yeye ni anahusika kwa vifo vya maelfu ya watu waliouawa wakati wa kuwania urais. Kama Wakenya wanataka kumuwajibisha mtu kwa uhalifu basi waanze kumuwajibisha yeye kwanza.

AJ: Watu wengi, ikiwa ni pamoja na Serikali za Somalia na Kenya, wanasema kuwa Al-Shabaab kulilenga eneo lililojaa raia ni dalili ya udhaifu, kwamba Al-Shabaab inaishiwa nguvu na kwamba inaelekea kutoweka kabisa na kubaki kuwa historia. Je hali iko hivyo?

SA: Ni watu gani hao wanaotuhukumu? Udhaifu wa hawa watu unaonekana kwa kila mtu. Serikali ya Somalia inalindwa na vifaru ili iendelee kuwa madarakani. Wakenya wanategemea msaada kutoka nje, hata kwenye kushughulikia suala dogo kama la Westgate. Waliomba msaada kutoka Magharibi.

AJ: Mwisho, Kenya imekielezea Kituo cha Vijana cha Mombasa Youth Centre (MYC) kwamba ni taasisi ya kigaidi. Katika maeneo mbalimbali kundi hilo limekuwa likiwaunga mkono Al-Shabaab. Al-Shabaab ina uhusiano gani na MYC?


SA: Uhusiano kati ya MYC na sisi ni kama uhusiano uliopo baina ya Waislamu. Wao ndugu zetu wa Kiislamu. Uhusiano uliopo ni kwamba wao ni Waislamu na sisi ni Waislamu, wana haki kutoka kwetu kama Waislamu wengine.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment