Piga vita tumbaku: zuia matangazo,uhamasishaji na udhamini wake


Mei 31, kila mwaka, yaani leo… ni siku ya kupinga matumizi ya tumbaku duniani. Shirika la Afya Duniani(WHO) na washirika wake wameitenga siku hii kuwa ni maalum kwa ajili ya kupiga vita matumizi ya sigara inayotengenezwa kwa tumbaku.
Katika siku hii elimu hutolewa kuhusu athari za kiafya zitokanazo na tumbaku na pia  kuwakilisha sera bora za namna ya kupunguza utumiaji wa tumbaku.
WHO linasema tumbaku inaua takribani watu milioni 6 kila mwaka na kati ya hao 600,000 sio wavutaji wa tumbaku. Mwaka huu ikiwa na kauli mbiu “fungia matangazo yanayotangaza, uhamasishaji na udhamini wa tumbaku.
Tumbaku ni hatari kwa afya na huleta madhara makubwa  katika maeneo mbalimbali ya mwili kama vile moyo,ini na  mapafu.
Uvutaji wa tumbaku unakuweka katika hatari ya kupata shambulizi la moyo, kiharusi,kikohozi sugu,mikwamo katika mirija ya kupitishia hewa,kuharibika tishu za mapafu, saratani hasa ya mapafu,koo na mdomo,pia madhara ya mishipa ya damu kuifanya kunyauka na kuwa myembamba hivyo kusababisha shinikizo la damu.
 Matumizi ya kilevi hiki ni hatari kwa mvutaji na yule aliye karibu na mvutaji. Madhara ya kiafya ni yaleyale, tofauti ni ndogo kuwa muathirika sana ni yule anaevuta. Kwa sababu hii, nchi mbalimbali duniani  zimepiga marafuku matumizi ya tumbaku katika maeneo yenye mkusanyiko wa watu; kama vile ndani ya vyombo vya usafiri,maeneo ya starehe na mikutano.
Je unayafamu Madhara ya tumbaku?
Utumiaji tumbaku huleta madhara kwa mwanamke kama vile ugumba, kijifungua kabla ya wakati, mimba kutoka na kuharibika, mtoto kufia tumboni, kuzaliwa na uzito mdogo.
 Moyo na ubongo
Utumiaji wa tumbaku husababisha mishipa ya damu kusinyaa/kuwa myembamba na kukamaa kwa mishipa ya damu inayopeleka damu katika misuli ya moyo, kuchochea mapigo ya moyo kwenda mbio na kuongezeka kwa lehemu (cholesteral). Matokeo ya haya ni kuharibika tishu za moyo,shambulizi la moyo, shinikizo la damu, ugonjwa wa kiharusi,ugonjwa wa kusahau kwa wavutaji wa umri mkubwa, upungufu wa uwezo wa kiakili, kushindwa kutambua na kupoteza kumbukumbu.
Mapafu
Kuharibika kwa tishu za mapafu na mirija ya hewa,madhahara yake ni Kikohozi sugu, mikwamo katika njia ya hewa,kushindwa kupumua vizuri, kupata maambukizi ya mara kwa mara ya vimelea vinavyoshambulia mfumo wa upumuaji na Saratani ya mapafu.
Taarifa za kitafiti kuhusu utumiaji tumbaku
Wataalamu wa saratani wanaeleza katika tafiti mbalimbali kuwa asilimia 30% za saratani zote hutokana na utumiaji tumbaki peke yake.Huku saratani ya mapafu ikiongezeka idadi kwa kina mama na kua….hii ni kutokana na taarifa ya utafiti uliofanyika nchini Uingereza,hii inatokana na wanawake wanaotumia tumbaku.Inakadiriwa kuwa 17.2% ya wanaume watumia tumbaku wako katika hatari yakupata saratani ya mapafu huku wanawake wakiwa ni 11.6%.
Tumbaki inasababisha vifo vya mapema ambavyo vinazuilika kama watu wasingeitumia,tafiti zinaonyesha kuharibika na kutoka kwa mimba kwa watumiaji tumbaku,pia watoto huzaliwa na uzito mdogo na pia kuzaliwa kabla ya mda kufika(njiti),Napia kuna hatari kwa zaidi ya 1.4 mpaka 3 yakupata vifo vya ghafla kwa mtoto aliye tumboni.
Tatafiti iliyofanyika kwa watoto wa panya wataalam wamegundua tumbaku  hupunguza uwezo wa ubongo wa mtoto kutambua hali ya hewa kua ndogo hivyo mtoto hupata jeraha la ubongo wakati wakuzaliwa. Uhanithi umeonekana kwa asilimia 85%  kwa watumiaj wa tumbaku ukilinganisha na wasiotumia, tumbaku ni moja ya kisababishi cha upungufu wa nguvu za kiume.
Tafiti nyingine ambayo ilichapishwa katika bbc health news ilisema kuongezeka kwa idadi ya wagonjwa wa saratani ya mapafu kwa upande wakina mama imeongezeka nakukaribia ya wanaume ukilinganisha na miaka ya nyuma hii imetokana na tabia mpya yakina mama kujiingiza katika utumiaji na uvutaji tumbaku
Tafiti nyingine ambayo ilifanyika nchini uingereza ilihusisha madaktari wakiume 34,486 nusu yao walikufa mapema kutoka na uvutaji sigara,wavutaji wako katika hatari ya kufa mapema kabla ya kufika umri wa miaka 60-70 mara 3 zaidi ukilinaganisha na wasiovuta.
Kwa nini tumbaki ni hatari kwa afya ya mwili?
 Tumbaku ina takribani kemikali 19 ambazo ni visababishi vya saratani,,na matokeo yake hujitokeza hata baadae maishani zaid ya maika 20
Tumbaku imebeba kemikali ambayo ni moja ya kisababishi cha saratani mwili, inaitwa pyrolitic,husababisha vitu vilivyomo ndani ya chembe hai kuvurugika, kitaalam genetic mutation. Mvurugiko huu ndio baadaye huleta saratani,pia tumbaku ina kemikali iitwayo nikotini ambayo husababisha uteja (addiction), husababisha mtu kuwa na utegemezi(dependency) wa kimwili na kiakili(saikologia) kwa tumbaku, hivyo mtu hushindwa kustahimili kutoikosa tumbaki na mtu huridhika pale anapoipata

 
Namna yakuacha na kijikinga na utumiaji tumbaku.
Zipo zaidi ya mbinu ishirini za namna yakuacha utumiaji tumbaku,kwanza unatakiwa kujichelewesha zaidi ya dakika kumi pale unapopata hamu yakuvuta tumbaku halafu fanya jambo lingine lolote ili kupoteza wazo la hamu ya uvutaji. Fanya hivi kwa mara nyingi zaidi. Jaribu kukwepa na kuvitambua vitu vinavyokushawishi kuvuta sigara kama vile kunywa pombe, kusikiliza mziki au kampani ya marifiki wanaovuta tumbaku.Mazoezi ya viungo vya mwili yanasaidia sana kupoteza wazo la kutamani tumbaku, kufanya mazoezi kwa dakika 30 kila siku inasaidia, pia unapokuwepo mahali km ofisini jaribu kunyoosha miguu, mikono, shingo mgongo, au hata kupiga ‘pushup’,pia kusali kufanya kazi ndogondogo km kufuma.
Share on Google Plus

About mahamoud

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment