HAMAS: ISRAEL IMEJIFUNGULIA MILANGO YA MOTO

NA KABUGA KANYEGERI

Harakati ya Hamas imesema kuwa Israel imejifungulia milango ya moto kwa hatua yake ya kumuua kamanda wa kijeshi wa Hamas  Ahmed Jabari katika Ukanda wa Gaza. 





Hamas, Gaza, Ahmed Jabari
Wapalestina wakizima moto kwenye gari la Ahmed Jabari
Bwana Jabari, ambaye alikuwa mkuu wa Brigedi ya al-Qassam, aliuawa katika shambulio lililolenga gari lake mjini Gaza, huku kwa uchache mtu mmoja akiuawa.

Umati mkubwa wa watu ulikusanyika kwenye eneo hilo baada ya mlipuko huo ulioacha shimo kubwa barabarani.

Israel ilisema kuwa kuuawa kwa Bwana Jabari, ambaye ni afisa mwandamizi wa ngazi ya juu wa Hamas kuuawa tangu kuvamiwa Gaza miaka minne iliyopita, ni mwanzo wa operesheni mpya dhidi ya wanaharakati hao.





Ahmed Jabari
Ahmed Jabari alikuwa mkuu wa tawi la kijeshi la Hamas
'Saa moja iliyopta, IDF ilimlenga Ahmed Jabari, kiongozi wa tawi la kijeshi la Hamas, katika Ukanda wa Gaza. Jabari alikuwa kiongozi mwandamizi wa Hamas aliyetumika katika ngazi ya juu ya jeshi la Hamas na alihusika moja kwa moja na mashambulizi dhidi ya Israel miaka kadhaa iliyopita,' ilisema taarifa ya Jeshi la Wazayuni.

Msemaji wa Jeshi la Wazayuni, Luteni Kanali Avital Leibovitch liongeza kusema kuwa shambulizi hilo ni 'mwanzo wa operesheni kubwa.'


'Lengo la operesheni hii ni kutatiza shughuli za kamandi hiyo na kudhibiti mlolongo wa uongozi wa Hamas na miundombinu yake. Hii ilikuwa operesheni kubwa iliyoshirikisha shirika la usalama la Israel, iliyotekelezwa kwa msingi wa intelejensia kubwa na kutumia uwezo wa hali ya juu,' ilieleza taarifa hiyo ya IDF.

Katika vita ya wiki tatu huko Gaza baina ya Desemba 2008 na Januari 2009, mamia ya watu waliuawa, wengi wao wakiwa raia wa kawaida, na maelfu ya nyumba kuharibiwa vibaya.






Hamas, Israel, Gaza
Israel inadai kuwa mauaji hayo ni mwanzo wa operesheni dhidi ya harakati ya Hamas
Israel imeendeleza mzingiro wa ardhini, angani na baharini dhidi ya Ukanda wa Gaza tangu Hamas iliposhinda uchaguzi wa bunge wa mwaka 2006, ikidai kuwa kuna ulazima wa kuzuia kuongezeka kwa mashambulizi ya roketi katika ardhi yake.
Kiongozi wa Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa na Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu iliuhesabu mzingiro huo kuwa wa haramu.
Bwana Jabari alikuwa katika orodha ya juu ya watu wanaotafutwa na Israel na alilaumiwa na Wazayuni hao kwa utekwaji wa askari wa Kiisrael Gilad Shalit mwaka 2006.

Hamas, ambayo siku za karibuni ilianzisha mashambulizi ya roketi kwenda Israel kwa kushirikiana na wanaharakati wengine wa kijeshi, iliripoti kufanyika kwa mashambulizi mengine matatu ya anga dhidi ya Gaza.

Share on Google Plus

About mahamoud

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment