HUYU NDIYE WAZIRI MKUU MPYA WA ETHIOPIA


 
Waziri Mkuu Mpya wa Ethiopia Hailemariam Desalegn ameapishwa kushika wadhifa huo, siku chache baada ya mazishi ya Waziri Mkuu wa zamani, Meles Zenawi yaliyofanyika katika mji mkuu wa nchi hiyo, Addis Ababa.

"Mimi, Hailemariam Desalegn, mbele ya bunge, ninakubali kuwa Waziri Mkuu wa Ethiopia... Kwa uamuzi wa Chama Cha Mapinduzi ya Kidemokrasia cha Watu wa Ethiopia (Ethiopian Peoples' Revolutionary Democratic Front -EPRDF) na bunge, nina furaha sana kuchukua jukumu la kuwa Waziri Mkuu...Tumeiletea nchi amani, demkrasia na maendeleo," Shirika la AFP lilimnukuu  Desalegn akitamaka hayo leo Ijumaa.


“Meles [waziri mkuu wa zamani] alikuwa akijihesabu kuwa mwana wa watu...Ninaahidi kuendeleza historia ya Meles bila kubadilisha chochote...Tutaimarisha demokrasia na haki za binaadamu nchini. Iwapo yatatokea matatizo tutayatatua...Tutafanya kazi pamoja na mashirika ya haki za binaadamu, tume ya uchaguzi na baadhi ya vyama vya upinzani," aliongeza.


Wiki iliyopita, wabunge walimteua mhandisi huyo wa maji mwenye umri wa miaka 47 kuwa mwenyekiti wa muungano wa chama cha Ethiopian Peoples' Revolutionary Democratic Front (EPRDF) na waziri mkuu wa nchi hiyo.
Mapema mwezi Agosti, Meles Zenawi [waziri mkuu wa zamani] alifariki dunia akiwa na umri wa miaka 57 katika hospitali moja nchini Ubelgiji na mwili wake kuzikwa katika makaburi ya Holy Trinity Cathedral katika mji mkuu wa nchi hiyo.

Wakati huohuo, ripoti zinasema kuwa sababu za kifo cha Zenawi bado hazijajulikana.

Zenawi, ambaye alikuwa madarakani tangu mwaka 1991, alisifika kwa ukuaji wa uchumi wa Ethiopia.
Share on Google Plus

About mahamoud

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment