WAPALESTINA WALAANI VITISHO VYA MAREKANI JUU YA MJI WA JERUSALEM

Palestinians blast US ‘coercion’ over Jerusalem
Msemaji wa Ikulu ya Palestina, Nabil Abu Rudeineh


JERUSALEM

Jerusalem is “haiuzwi”, Maafisa wa Kipalestina wamesema wamesema leo Jumatano baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kutishia kuikatia misaada ya kifedha serikali ya Mamlaka ya Palestina iwapo haitaanza mazungumzo na utawala wa Israel.

“Jerusalem haiuzwi, si kwa dhahabu wala fedha,” msemaji wa Rais wa Palestina, Nabil Abu Rudeineh amesema katika taarifa iliyorushwa na shirika rasmi la habari la Palestina, WAFA.

“Kama Marekani ina wasiwasi na maslahi yake katika eneo la Mashariki ya Kati, inapaswa kufungamana na misingi na rejea za Baraza la Usalama na Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa,” amsema Abu Rudeineh.

“Vinginevyo, Marekani itaishia kulitumbukiza eneo hili shimoni,” aliongeza.

Abu Rudeineh amesema kuwa uongozi wa Palestina haupingi kurudi kwenye meza ya mazungumzo, bali “mazungumzo ya kweli yanatakiwa kuwa na uhalali wa kimataifa na mpango wa amani wa jumuiya ya Kiarabu [mpango wa mwaka 2002 unaoungwa mkono na Saudi Arabia], ambao unatoa wito wa kuundwa kwa taifa huru la Palestina huku mji mkuu wake ukiwa Jerusalem Mashariki."

Naye msemaji wa vuguvugu la Hamas, Fawzi Barhoum, amekielezea kitisho cha Trump kama "kitisho rahisi cha kisiasa."

"Vitisho hivi vinaakisi tabia ya kinyama na utovu wa maadili wa Marekani katika kuamiliana na madai ya Palestina na Wapalestina," amesema Barhoum katika taarifa yake mapema leo Jumatano.

“Ili kukabiliana na shinikizo hili la Marekani kunahitajika juhudi kubwa zaidi ili kufanikisha umoja wa Wapalestina,” aliongeza. 

Msemaji huyo wa Hamas aliendelea kusisitiza hitajio la kuiunganisha “misimamo ya Waarabu, Waislamu na Jumuiya ya Kimataifa katika kuunga mkono haki za Wapalestina dhidi ya matendo ya Marekani na utawala wa Wazayuni wa Israel."

Hanan Ashrawi, mwanazuoni wa Kipalestina na mjumbe wa Kamati Tendaji ya Chama cha Ukombozi wa Palestina (PLO), kwa upande wake alisisitiza msimamo kwamba haki za Wapalestina “haziuzwi”.

“Kwa kitendo cha kuutambua mji wa Jerusalem unaokaliwa kimabavu kama mji mkuu wa Israel, sio tu kwamba Trump amekwenda kinyume na sheria ya kimataifa, bali pia amevuruga mchakato wa amani huku akichochea vitendo haramu vya utawala wa Israel kuumega mji wetu mkuu,” Ashrawi amesema katika taarifa yake.

“Hatutatishika,” alisema. “Trump amehujumu amani, haki na uhuru ambao tumekuwa tukiutafuta na sasa anatutisha kutuadhibu kwa matokeo ya sera yake iliyokosa akili."


Mnamo Desemba 6, Trump alitangaza uamuzi wake wa kuutambua mji wa Jerusalem kama mji mkuu wa utawala wa Israel, hatua iliyosababisha maandamano makubwa na lawama kutoka ulimwengu wa Kiarabu na Kiislamu.

Tangu wakati huo, kwa uchache Wapalestina 15 wameuawa – na maelfu kujeruhiwa – katika makabiliano makali na vikosi vya utawala wa Israel.

Mapema siku ya Jumanne, rais wa Marekani alitishia kukata msaada wa kifedha kwa serikali la Mamlaka ya Palestina yenye makao yake mjini Ramallah.

"Tunawalipa Wapalestina maelfu kwa mamilioni ya dola kila mwaka na badala yake hawatushukuru au kutuheshimu," aliandika Trump kwenye mtandao wa twitter.

"Hawataki hata kufanya mazungumzo kuhusu amani ya kudumu na Israel,” alisema. “Tumeitwaa Jerusalem, nje ya meza ya mazungumzo, kipengele ambacho kilikuwa kigumu zaidi katika mazungumzo, lakini Israel, kwa hilo, ingelipa gharama kubwa.”

“Kwa kuwa Wapalestina hawataki tena kuzungumzia amani, kwa nini tuendelee kuwalipa mapesa mengi kiasi hiki? " alihoji.

Awamu ya mwisho ya mazungumzo ya amani kati ya Israel na Palestina ilivunjika mwaka 2014 baada ya Israel kukataa kuliachia huru kundi la wafungwa wa Kipalestina licha ya kutoa ahadi hiyo mapema.


Mji wa Jerusalem umeendelea kuwa kitovu cha mgogoro wa Mashariki ya Kati,  huku Wapalestina wakitumai kwamba Jerusalem ya Mashariki—inayokaliwa kimabavu na Israel tangu mwaka 1967 – itakuwa mji mkuu wa taifa huru la Palestina.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment