WENGER: SANCHEZ HAJAOMBA KUONDOKA

Image result for Arsene Wenger press in Australia

Arsene Wenger ametupilia mbali ripoti kuwa Alexis Sanchez ameiambia Arsenal kuwa anataka kuondoka katika msimu huu wa majira ya joto.

Wenger alitoa kanusho la mkato na la moja kwa moja alipoulizwa kuhusu tetesi kuwa mchezaji huyo alimtaarifu azma yake ya kutaka kuondoka kwenye klabu hiyo yenye makao yake kaskazini mwa jiji la London katika juhudi zake za kutaka kucheza michuano ya Ligi ya Mabingwa katika klabu ya Manchester City.

Meneja huyo wa muda mrefu aliendelea kutokuwa wazi kuhusu mustakbali wa Sanchez licha ya tetesi zilizozagaa zikimhusisha nyota huyo mwenye umri wa miaka 28 kwamba anataka kuungana na kocha wa zamani wa Barcelona Pep Guardiola katika dimba la Etihad.

Hilo limewapelekea watu wengi kuamini anaweza kuendelea kubaki Arsenal mpaka mwishoni mwa mkataba wake licha ya kwamba amekataa kusaini mkataba mpya na klabu hiyo ya dimba Emirates.

Wenger ambaye yuko mjini Sydney kwa ajili ya michezo miwili ya kirafiki na kilabu za ligi kuu ya nchi hiyo, A-League, za Sydney FC na Western Sydney, amesisitiza azma yake ya kutomuuza Sanchez kwa mahasimu wao wa Ligi Kuu ya Uingereza.

"Hakuna ajuaye leo kama Sanchez atakuwa katika mwaka wa mwisho wa mkataba wake, kwa sababu anaweza kuongeza mkataba wake na sisi mwanzoni mwa msimu au katikati ya msimu," Wenger alisema.

"Hivyo, sio lazima huu uwe mwaka wa mwisho wa mkataba wake kwenye klabu ya Arsenal."

Sanchez ameachwa katika safari hiyo ya Australia baada ya kuichezea timu yake ya taifa la Chile kwenye michuano ya Kombe la Mabara iliyomalizika hivi karibuni nchini Urusi.

Image result for Alexis Sanchez

Mchezaji mwingine aliyezungumzwa sana, Olivier Giroud, ameungana na kikosi hicho katika safari yake ya Sydney.

Straika huyo raia wa Ufaransa anaelezwa kuwa anawindwa na vilabu vya Everton, Marseille na West Ham.

Giroud alipoteza nafasi yake katika kikosi cha kwanza kwa sehemu kubwa ya msimu uliopita ambapo nafasi yake ilichukuliwa na Sanchez na wakati mwingine Danny Welbeck, jambo lililomfanya kueleza kuwa anataka kuchezezwa mara kwa mara.

Kuwasilia kwa Alexandre Lacazette kunaweza kupunguza zaidi ushiriki wake dimbani, lakini Wenger amesisitiza kuwa Giroud, ambaye aliongeza mkataba wake mwezi Januari, ni mchezaji muhimu kwa kikosi chake.

Bosi huyo wa Arsenal alithibitisha kuwa Lacazette atashiriki katika mchezo wa Alhamisi dhidi ya Sydney FC kabla ya kipute cha Jumamosi dhidi ya Western Sydney.
"Ndiyo, Lacazette ataanza kucheza hapa" alisema Wenger.
"Bila shaka Alhamisi usiku atashiriki mchezoni. Atacheza mechi zote mbili."

Usajili wa mchezo huyo mwenye umri wa miaka 26, ambaye alifunga magoli 100 kwenye michezo 203 aliyocheza na klabu ya Lyon katika ligi kuu ya Ufaransa, Ligue 1, ni mapinduzi kwa Wenger ambaye klabu yake imeshindwa kuingia katika nafasi nne za juu na kushindwa kufuzu kwa michuano ya Klabu Bingwa katika hatua ambayo inaonekana kuwa ni zama mbaya kabisa katika kipindi chote cha kazi ya ukocha kwa miaka 21.

Mchezaji mwingine aliyesajiliwa hivi karibuni, raia wa Bosnia-Herzegovina, Sead Kolasinac, naye amesafiri na klabu na anaweza kucheza katika ziara hiyo ya kwanza nchini humo kwa kipindi cha miaka 40, kabla ya kuendelea na ziara ya kujiandaa na msimu mpya watakayoifanya nchini China.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment