SHAMBULIZI LAUA NA KUJERUHI KADHAA MJINI KABUL

Smoke is seen after a powerful explosion in central Kabul, April 19, 2016.
Moshi ukionekana baada ya shambulizi kubwa kuutikisa mji wa Kabul nchini Afghanistan leo Aprili 19, 2016

Watu wengi wameuawa na wengine kujeruhiwa katika mlipuko uliotokea katikati ya mji wa Kabul, Afghanistan mapema leo asubuhi, Rais Ashraf Ghani amesema.

Kituo cha televisheni chan Tolo News cha nchini humo kimesema kuwa kwa uchache watu 28 wameuawa na wengine zaidi ya 200 wamejeruhiwa katika shambulizi hilo lililoratibiwa.

Shambulizi hilo, lililodaiwa kutekelezwa na wanamgambo wa Taliban, lililenga ofisi za idara kuu ya usalama ya nchi hiyo.

katika taarifa yake, ikulu ya nchi hiyo imelaani vikali shambulizi hilo na kusema kuwa watu kadhaa wameuawa au kujeruhiwa.

Msemaji mmoja wa hospitali ya huduma za dharura mjini humo ameliambia shirika la habari la Reuters kuwa hospitali yake imepokea askari 8 wa Kiafghan waliojeruhiwa.


Wanamgambo wa Taliban waliongeza mashambulizi dhidi ya vikosi vya kigeni na vile vya serikali ya Afghanistan tangu walipotangaza kuanza mashambulizi waliyoyaita kama “mashambulizi ya machipuo” wiki iliyopita.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment