SAUDI ARABIA YAWANYONGA WATU 47 KWA HATIA ZA UGAIDI

In this Sunday, Sept. 30, 2012 file photo, a Saudi anti-government protester carries a poster with the image of Shiite cleric Sheik Nimr al-Nimr (AP Photo, File)
Picha hii iliyochukuliwa Septemba 30, 2012 ikiwaonesha waandamanaji wanaoipinga serikali wakiwa wamebeba bango lenye picha ya kiongozi wa Washia nchini humo, Nimr Al-Nimr.

Leo Saudi Arabia imewanyonga watu 47 waliokutwa na hatia ya “ugaidi”, akiwemo kiongozi mkubwa wa kidini wa madhehebu ya Kishia anayedaiwa kuchochea maandamano dhidi ya serikali, wizara ya mambo ya ndani imesema.

Kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 56, Nimr al-Nimr, alikuwa mhamasishaji wa maandamano yaliyoibuka mwaka 2011 katika eneo la mashariki ya nchi hiyo yenye Wasunni wengi, ambapo Washia wachache wanalalamika kuwa wanabaguliwa.

Lakini orodha hiyo haijumuishi mpwa wa Nimr, Ali al-Nimr, ambaye alikuwa na umri wa miaka 17 alipokamatwa kufuatia maandamano hayo.

Taarifa hiyo ya wizara, iliyorushwa na shirika la habari la nchi hiyo (SPA), imesema kuwa watu hao 47 walitiwa hatiani kwa kasumba za misimamo mikali, kujiunga na makundi ya kigaidi na kutekeleza njama mbalimbali za kihalifu.

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Iran, Hossein Jaber Ansari, amesema kuwa Saudi Arabia italipa “gharama kubwa” kwa kumnyonga Nimr al-Nimr.

"Serikali ya Saudia inakabiliana na wakosoaji wa ndani kwa kutumia mabavu na mauaji… serikali ya Saudia italipa gharama kubwa kwa kufuata sera hizo,” alisema Ansari, aliyenukuliwa na shirika la habari la Iran (IRNA).

Kunyongwa kwa Nimr kunaweza kuchochea ghadhabu ya vijana wa kishia, kakaye alionya, huku akitaka kuwepo kwa utulivu.

"Hatua hii itawasha hasira za vijana (wa Kishia)” nchini Saudi Arabia, alisema Mohammed al-Nimr, na kutaka kuwepo kwa vuguvugu la upinzani wa amani.


"Tunakataa ghasia na makabiliano na serikali,” alisema.

Aidha, orodha hiyo inajumuisha Wasunni waliotiwa hatiani kwa kuhusika na mashambulizi ya Al-Qaeda yaliyoua Wasaudia na raia wa kigeni katika taifa hilo mwaka 2003 na 2004.

Walionyongwa ni pamoja na raia mmoja wa Misri na mwingine wa India. Wengine wote walikuwa Wasaudia.

Orodha hiyo inamjumuisha Fares al-Shuwail ambaye vyombo vya habari nchini humo vinamuelezea kuwa kiongozi mkuu wa kidini wa kundi la Al-Qaeda nchini Saudi Arabia. Alikamatwa Agosti 2004.

Wizara imesema kuwa walinyongwa katika maeneo 12 tofauti katika miji mbalimbali ya taifa hilo, bila kutoa maelezo ya kina juu ya njia zilizotumika kuwanyonga.

Kwa kawaida unyongaji nchini humo hufanyika kwa kukata vichwa vya wahusika kwa kutumia panga.

Adhabu za unyongaji zimeongezeka nchini humo tangu Mfalme Salman alipokalia kiti cha ufalme Januari 2015 kufuatia kifo cha mfalme Abdullah.

Idadi ya walionyongwa leo ni zaidi ya nusu ya wale walionyongwa katika kipindi cha mtangulizi wa Salma kwa mwaka wote wa 2014 ambao ni 87.

Mwaka 2015, Saudi Arabia iliwanyonga watu 153 waliokutwa na hatia ya makosa mbalimbali, ikiwemo usafirishaji wa madawa ya kulevya.

Mwaka 2011, mamlaka za nchi hiyo ziliweka mahakama maalumu zinazoshughulikia kesi za raia na wageni wanaoshukiwa kuwa wafuasi wa kundi la Al-Qaeda au walioshiriki katika wimbi la mashambulizi yaliyoikumba nchi hiyo tangu mwaka 2003.

Mashambulizi hayo yaliwaua zaidi ya askari 150 wa nchi hiyo na raia wengine wa kigeni.

Mwanamfalme wa sasa anayetarajiwa kukalia kiti cha ufalme, Mohammed bin Nayef,  alisimamia zoezi la kuwashughulikia wanamgambo wakati huo.

Lakini Nimr alikamatwa kwa sababu tofauti mwaka 2012.
Wakati huo wizara ya mambo ya ndani ilimuelezea kama mchochezi na kutangaza kuwa amekamatwa katika kijiji cha Washia cha Awamiya mashariki mwa nchi hiyo baada ya kujeruhiwa mguuni wakati akipinga kukamatwa.




Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment