ARSENE WENGER: NITAIMARISHA KIKOSI CHANGU MWEZI JANUARI

 arsene wenger


Kocha wa klabu ya Arsenal, Arsène Wenger, amesema kuwa anapanda na kushuka ili kukiimarisha kikosi chake katika dirisha la usajili litakalofunguliwa mwezi Januari.

Meneja huyo wa washika bunduki wa Emirates ana upuungufu kwenye eneo la kiungo kufuatia kujeruhiwa kwa Francis Coquelin, Santi Cazorla, Jack Wilshere, Tomas Rosicky na Mikel Arteta.

“Hakika nitafanya kazi kubwa,” amesema Wenger. “Nimeshakuwa na kazi kubwa na nilisema mwezi mmoja uliopita kuwa tuna upungufu kwenye mashindano yote tunayokutana nayo, hususani kwenye eneo la kiungo. Naam, tutafanya kazi kubwa.”

Arsenal imehusishwa na uhamisho wa kiungo wa FC Basel, Mohamed Elneny, huku Wenger akikiri kuwa Mathieu Debucky anaweza kuondoka Emirates.

“Kwa bahati mbaya hatuwezi kutangaza chochote kwa sasa kuhusu mchezaji huyu [Elneny] kwa sababu hakuna chochote kilichofikiwa,” alisema.

“Sio kwamba haiwezekani [kwa Debuchy kuondoka]. Nitafurahi kama akibaki, lakini tusubiri.”


CHANZO: Arsenal.com
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment