MURSI: NIMENUSURIKA KUPEWA SUMU

A file picture taken on June 2, 2015 shows ousted Egyptian President Mohamed Morsi gesturing from the defendants cage as he attends a trial at the police academy on the outskirts of the capital, Cairo. (AFP photo) 


Rais wa Misri aliyeondolewa madarakani, Mohammed Morsi, amesema kuwa lilifanywa jaribio la kumlisha sumu gerezani anakoshikiliwa.

Mapema jana, Morsi alisema kuwa alikataa kula chakula cha magereza alichopewa tarehe 21 na 22 Julai kwa hofu ya kulishwa sumu.

“Kama ningekula, jinai ingetokea,” alisema wakati vikao vya mahakama vilivyoanza siku hiyo katika mashitaka yanayomkubali ambapo anashitakiwa kuvujisha siri za usalama wa taifa.

Morsi alisema kuwa kwa uchache matukio matano yalitokea na yangehatarisha maisha yake iwapo yangefanikiwa.

Aidha, aliitaka mahakama impatie uwezo wa kuhudumiwa na madaktari wake kwa kuwa anasumbuliwa na tatizo la sukari.

Morsi alikuwa rais wa kwanza kuchaguliwa kidemokrasia nchini Misri, na alipinduliwa na aliyekuwa mkuu wa jeshi la nchi hiyo Abdul-Fattah Al-Sisi Julai 2013. Al-Sisi ndiye rais wa sasa wa Misri.

Mwezi jana, mahakama ilimhukumu Mursi adhabu ya kifo kwa tuhuma za kuvujisha taarifa za usalama na kusaidia watuhumiwa kutoroka jela. Mursi na wafuasi wake wamekataa tuhuma hizo na kusema kuwa zimechochewa kisiasa.



Tangu kupinduliwa kwa Mursi, Misri imeshuhudia ghasia ambazo zilisababisha watu wengi kupoteza maisha.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment