VIONGOZI WA ACT WAZALENDO ZIARANI NCHINI UJERUMANI



Viongozi wa ACT Wazalendo safarini Ujerumani kwa mwaliko wa chama cha Die Linke

Mwenyekiti wa chama cha act wazalendo mama Anna Mghwira akiongozana na katibu mkuu Ndugu samson mwigamba na katibu wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa ndugu Venance Msebo leo tarehe 15 julai 2015 wameanza ziara ya siku saba nchini ujerumani kwa mwaliko wa chama rafiki cha kijamaa (Die Linke Party).

Katika ziara hiyo pamoja na kutembelea die linke party, watapata fursa ya kutembelea ubalozi wa Tanzania nchini Ujerumani na pia watafanya mkutano na watanzania wanaoishi nchini ujerumani katika kuwahamasisha kuchangia maendeleo ya nchi yao na pia kutafuta fursa kurudi nyumbani kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura pamoja na kupiga kura ifikapo Oktoba mwaka huu.

Imetolewa na afisa habari,

Act wazalendo

Abdallah Khamis


15 julai 2015
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment