Mwanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Muslim Hassanali akirudisha fomu kwa Mratibu wa Kanda ya Pwani, Casimir Juma Mabina za kuomba kuteuliwa kuwa mgombea ubunge kwa tiketi ya chadema katika uchaguzi mkuu ujao. Kulia ni Mjumbe wa Kamati Kuu Chadema, Mabere Marando. (Picha na Francis Dande)
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mabere Marando (kushoto) akimkabidhi kadi ya Chama hicho aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM tawi la Kigamboni Wilaya ya Mafia, Mohamed Makungu ambaye amekiama chama chake na kujiunga na Chadema. Hafla hiyo ilifanyika katika Ofisi za Kanda ya Pwani jijini Dar es Salaam jana. Katikati ni Mwenyekiti Bodi ya Wadhamini wa chama hicho, Arcado Ntagazwa.
0 comments:
Post a Comment