JESHI LA SUDAN KUSINI KATIKA KASHFA YA KUWAUA NA KUWACHOMA MOTO MABINTI WAKIWA HAI

A photo, taken on January 26, 2014, shows South Sudanese government soldiers riding in a pickup truck. (AFP photo)
Askari wa Jeshi la serikali ya Sudan Kusini


Umoja wa Mataifa (UN) umelituhumu jeshi la Sudan Kusini kwa vitendo vya kuwabaka na kuwachoma moto mabinti wakati wa mapambano ya hivi karibuni katika jimbo moja la mpakani.

Wachunguzi wa kikosi cha Umoja huo nchini Sudan (UNMISS) wameeleza hayo katika ripoti iliyochapishwa leo Jumanne.

Ripoti hiyo imetokana na ushuhuda wa waathirika na mashuhuda 115 kutoka katika jimbo la Unity kaskazini mwa nchi hiyo.

Jimbo hilo lipo kaskazini mwa Sudan Kusini, karibu na mpaka wa nchi hiyo na Jamhuri ya Sudan.

Hivi karibuni eneo hilo limeshuhudia mapigano makali kabisa tangu kuibuka kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyodumu kwa miezi 18 katika taifa hilo changa kabisa ulimwenguni.

UN imesema kuwa mapigano hayo, hususan katika wilaya ya Mayom aambayo ilikuwa eneo muhimu la uzalishaji wa mafuta, yalizuka mwezi Aprili baina ya vikosi vya serikali na waasi.

“Manusura wa mashambulizi haya waliripoti kuwa askari wa serikali na waasi kutoka wilaya ya Mayom waliendesha kampeni dhidi ya wakaazi ambayo iliwaua raia, kuharibu vijiji na kuwafanya zaidi ya watu 100,000 kuyakimbia makazi yao,” imesema ripoti hiyo.

“Baadhi ya tuhuma mbaya kabisa zilizokusanywa na maafisa wa UNMISS zilijikita kwenye utekaji na dhulma za ngono dhidi ya wanawake na mabinti, baadhi yao wakiripotiwa kuchomwa moto wakiwa hai katika makazi yao,” iliongeza.

Hata hivyo, jeshi la Sudan Kusini halijajibu tuhuma hizo. Huko nyuma nchi hiyo iliwahi kukanusha madai ya ripoti kama hizo.

UN imesema kuwa ripoti hiyo imekabidhiwa kwa maafisa wa serikali, ambao hawajaeleza chochote kuhusu utafiti huo.

Watoto wakimiminika katika eneo la ugawaji chakula katika jimbo la Unity, Sudan Kusini.

Sudan Kusini ilitumbukia katika ghasia mwezi Desemba mwaka 2013, baada ya mapigano kuzuka baina ya askari watiifu kwa Rais Salva Kiir na waasi wanaoongozwa na aliyekuwa makamu wa rais wa nchi hiyo, Riek Machar, katika mji mkuu Juba.

Ghasia hizo zimesababisha vifo vya maelfu ya watu na mamilioni wengine kuyakimbia makazi yao.


Sudan Kusini ilipata uhuru wake Julai 2011 baada ya raia wake kupiga kura kwa wingi kujitenga na Sudan.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment