WILLIAN AITAKATISHA CHELSEA LIGI KUU ENGLAND

BAO la dakika za lala salama la Willian, limeipa Chelsea ushindi wa 1-0 dhidi ya Everton usiku huu katika mcheo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Stamford Bridge, London.
Toffees walifungwa bao hilo baada ya kumpoteza mchezaji wake, Gareth Barry aliyetolewa kwa kadi nyekundu na sasa The Blues wanaendelea kuongoza Ligi Kuu kwa pointi saba zaidi.
Steven Naismith alikuwa mwenye bahati baada ya kuepuka adhabu licha ya kuunawa mpira kwenye boksi la Everton kipindi cha kwanza. 
Kiungo mpya, Juan Cuadrado alianza kwa amra ya kwanza leo tangu asajiliwe kwa Pauni Milioni 27 Chelsea kutoka Fiorentina na akavutia.
Willian is jubilant as he celebrates his late winner with substitute Didier Drogba, sending Stamford Bridge into pandemonium in the process
Willian akishangilia na Didier Drogba baada ya kufunga
Share on Google Plus

About mahamoud

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment