WAZIRI WA MICHEZO: SIJAWAHI KUTAZAMA MECHI YOYOTE

Waziri wa Michezo wa Mauritania Fatma Fal Bent Assouina Assouina.



Waziri mpya wa michezo nchini Mauritania amedai kuwa hajawahi kutazama mechi yoyote ya michezo na havielewi vifaa vya michezo muhimu, amenukuliwa na tovuti ya habari ya al Quds leo.

“Ninalazimika kutazama mechi hali ya kuwa sikuwahi kutazama mchezo wowote katika maisha yangu yote,” Fatma Fal Bent Assouina Assouina alimwambia mmoja wa mashabiki wake aliyekwenda kumpongeza baada ya kuteuliwa kushika wadhifa huo.

Assouina, ambayeni mwanamke wa nne kushika wadhifa huo, amemrithi Lalat Bint Asharif, ambaye alishika nafasi hiyo kwa kipindi kisichozidi miezi 8.


Sekta ya michezo nchini Mauritania imekuwa ikikabiliwa na changamoto nyingi kutokana na ukosefu wa ustadi wa mawaziri mbalimbali wanaoteuliwa kwenye sekta hiyo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment