MAZUNGUMZO YA AMANI YA SYRIA YAHITIMISHWA BILA NATIJA

UN envoy for Syria Lakhdar Brahimi speaks during a press conference on the Syrian peace talks at the United Nations headquarters on February 13, 2014 in Geneva.
Mjumbe wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Syria, Lakhdar Brahimi, akizungumza na waandishi wa habari juu ya mazungumzo ya amani ya Syria kwenye ofisi za Umoja wa Mataifa mjini Geneva Februari 13, 2014. 



Awamu ya pili ya mazungumzo ya kusaka amani yaliyokuwa yakifanyika mjini Geneva baina ya serikali ya Syria na wapinzani yamemalizika bila kupatikana matokeo ya moja kwa moja.

Hayo yamesemwa na msuluhishi wa kimataifa kwenye mgogoro huo, Lakhdar Brahimi.

Akizungumza na waandishi wa habari juu ya mazungumzo hayo, Bwana Brahimi alisema:

"Ninafikiri ni bora kwa kila upande kwenda kutafakari juu ya wajibu wao, na kujua iwapo wanataka mchakato huu uendelee au la.”

Naye mjumbe wa upinzani, Ahmad Jakal, amesema kuwa mwisho wa kikao hicho hawakuafikiana juu ya tarehe ya kuendelea na awamu ya tatu ya mazungumzo hayo:

"Kilikuwa kikao cha muda mfupi na kizito, kilichotawaliwa na tofauti kuhusu jinsi ya kushughulikia masuala la ghasia na serikali ya mpito. Brahimi hakupanga tarehe maalumu kwa ajili ya awamu ya tatu lakini aliweka wazi kuwa anatarajia kutakuwa na awamu nyingine ya mazungumzo,” alisema.

Mgogoro wa Syria umegharimu maisha ya watu zaidi ya 100,000 tangu Machi 2011.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment