WATU 90 WAUAWA NIGERIA

Nigerian soldiers patrol in the north of Borno state close to a Islamist extremist group Boko Haram former camp, file image from 2013
Eneo la Kaskazini mwa Nigeria limewekwa katika hali ya hatari, lakini mashambulizi yameendelea kugharimu maisha ya wakazi wa eneo hilo.

Watu wanaodaiwa kuwa wapiganaji wa kundi la Boko Haram la nchini Nigeria wamewaua watu wasiopungua 90, wakiwemo watoto na wanawake, katika shambulizi kwenye kijiji kimoja kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.

Kwa mujibu wa mashuhuda, shambulizi hilo limetokea katika kijiji cha Izghe katika jimbo la Borno leo hii.

Mashuhuda hao wanasema kuwa wanamgambo wenye silaha na mabomu, walikizunguka kijiji hicho na kukishambulia kwa risasi. Aidha, inadaiwa kuwa walizichoma moto nyumba kadhaa.

“Wakati huu ninapozungumza na wewe, maiti za watu waliouawa bado zimelala mitaani,”  mkazi wa kijiji hicho, Abubakar Usman alisema na kuongeza: “tulikimbia kuwazika, kwa hofu kwamba wauaji bado wanasabiri porini.”

Kamishna wa polisi katika jimbo la Borno, Lawal Tanko, amethibitisha kutokea kwa shambulizi hilo lakini akasema kuwa maelezo ya kina juu ya shambulizi hayo hayajathibitishwa.

Shambulizi hilo ni jipya kabisa katika mfululizo wa wimbi la ghasia katika eneo hilo la kaskazini mashariki mwa Nigeria.

Mnamo Januari 26, wanamgambo wakiwa na mabomu na silaha nyingine, walikishambulia kijiji cha Kawuri katika jimbo la Borno katika siku ya gulio.


Kwa mujibu wa wanausalama, katika tukio hilo watu 52 waliuawa na kijiji kuchomwa moto.

Siku hiyo hiyo, wanamgambo walilichoma kanisa moja katika kijiji cha Wada Chakawa katika jimbo la Adamawa. Walifyatua mabomu na kuyatupa kanisani, yakaua watu kadhaa, kabla ya kuzichoma nyumba na kuwachukua wakaazi wa kijiji hicho kama mateka katika mzingiro huo uliodumu kwa muda wa saa tano.

Mwenyekiti wa kijiji,  Maina Ularamu alisema kuwa polisi walikusanya miili 45, ikiwemo ya maafisa wawili wa polisi.

Mnamo Mei 2013, Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan, alitangaza hali ya hatari katika majimbo matatu kaskazini mashariki mwa nchi hiyo, ambayo ni Borno, Yobe, na Adamawa. Takwimu za Umoja wa Mataifa zinaonesha kuwa zaidi ya watu 1,200 wamepoteza maisha katika ghasia nchini humo tangu hali hiyo ya hatari ilipotangazwa.

Kundi la Boko Haram – yaani “Taaluma kutoka Magharibi ni Haramu” – linasema kuwa lengo lake ni kuiondosha serikali ya Nigeria.

Kundi hilo linadai kuhusika na mashambulizi kadhaa katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo tangu mwaka 2009.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment