RATIBA YA BUNGE LA KATIBA





Kwa mujibu wa Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah, Bunge la Katiba litaanza shughuli zake rasmi kesho kwa kusomwa kwa tangazo la kuitishwa kwa Bunge Maalumu la Katiba la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Siku hiyo pia kutafanyika uchaguzi wa mwenyekiti wa muda ambaye kazi yake kubwa itakuwa ni kuandaa kanuni za Bunge Maalumu la Katiba ambalo litakuwa na wajumbe 629.

Alisema baada ya kupatikana kwa kanuni, Ijumaa kutafanyika uchaguzi wa mwenyekiti na makamu wake kwa kuzingatia sheria ya Mabadiliko ya Katiba iliyopitishwa mwaka jana.

Alidokeza kwa kusema pia kuwa wateuliwa, Katibu na msaidizi wake wa Bunge hilo na kwa mujibu sheria hiyo, ataanza kazi baada ya kuapishwa na Rais na baada ya kuapishwa naye atamwapisha mwenyekiti wa Bunge hilo.


Baada ya mwenyekiti kuapishwa, atawalisha kiapo wajumbe wengine wa Bunge hilo, kazi ambayo itafanyika kwa siku tatu hadi Jumatatu asubuhi na mchana wake, Rais Kikwete atalizindua rasmi.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment