RAIS WA JAMHURI YA AFRIKA YA KATI ATANGAZA VITA DHIDI YA WANAMGAMBO

 
Kijana akiwa amekamata kisu katika mji mkuu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, Bangui, Februari 10, 2014.


Rais wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, Bi. Catherine Samba-Panza amesema kuwa serikali yake “itaingia vitani” dhidi ya wanamgambo wanaofanya mauaji dhidi ya raia wenzao Waislamu nchini humo.

Katika hotuba yake aliyoitoa jana, alisema kuwa: “wanamgambo wanadhani kuwa kwa sababu mimi ni mwanamke basi nitakuwa dhaifu. Sasa (wanamgambo wa) ant-Balaka, ambao wanataka kufanya mauaji, watawindwa na kusakwa.”

Rais Samba-Panza aliongeza kuwa wanamgambo hao wamepoteza maana ya harakati yao na kugeuka kuwa wauaji, wanyang’anyi na kueneza ghasia.

Taifa hilo lenye watu wapatao milioni 4.6 lilifubikwa na ghasia za kidini baina ya Wakiristo na Waislamu mwaka jana.

Hapo jana shirika la Amnesty International lilitoa ripoti yake likisema kuwa kuna mauaji ya kiholela yanayoendeshwa dhidi ya jamii ya Kiislamu nchini humo huku walinda amani wa kimataifa wakishindwa kuyakomesha.

Shirika hilo la haki za binadamu limesema kuwa limeorodhesha kwa uchache mauaji 200 dhidi ya Waislamu yaliyofanywa na wanamgambo wa Kikristo katika eneo la magharibi la nchi hiyo.

"Mauaji ya kiholela dhidi ya jamii ya Kiislamu yamekuwa yakifanyika katika eneo la magharibi la Jamhuri ya Afrika ya Kati, ambalo ndilo lenye wakazi wengi zaidi nchini humo, tangu mapema Januari 2014,” Amnesty imesema na kuongeza: “Jamii zote za Kiislamu zimelazimika kukimbia, na maelfu ya raia Waislamu, ambao hawakufanikiwa kutoroka, wameuawa na wanamgambo waliojipanga wa anti-Balaka.”

Zaidi ya watu 1,000 wameuawa katika Jamhuri ya Afrika ya Kati tangu mwezi Desemba baada ya wanamgambo wa Kikristo kufanya mashambulizi yaliyoratibiwa dhidi ya kundi la Seleka lenye Waislamu wengi, ambalo liliiangusha serikali mwezi Machi mwaka 2013.

Umoja wa Afrika umeshatuma kikosi askari 5,400 kati ya 6,000 wanaotakiwa kusaidia kutuliza ghasia hizo. Askari wengine 1,600 kutoka Ufaransa wameshatua katika nchi hiyo.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment