70 WAUAWA KATIKA MAPIGANO MAPYA JAMHURI YA AFRIKA YA KATI

Mwanamke akikimbia kutafuta hifadhi baada ya mapigano kuzuka katika wilaya ya Miskin, katika mji mkuu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, Bangui.



Watu sabini wameuawa katika awamu mpya ya makabiliano na ghasi zinazoendelea kuitikisa Jamhuri ya Afrika ya Kati.

Kamishna wa Pilisi nchini humo, Elie Mbailao, amesema leo kuwa ghasia hizo mbaya zimetokea katika mji wa Boda, kilometa 100 (maili 62) magharibi mwa mji mkuu, Bangui.

Kwa mujibu wa Kamanda Mbailao, mapigano hayo yaliyogeuka kuwa ghasia za kidini, yameshuhudia nyumba 30 kuchomwa moto katika mji huo.

Mapigano hayo yanatokea huku kukiwa na vikosi vya kulinda amani  kutoka Ufaransa na vile vya Umoja wa Afrika, lakini vikosi hivyo vimeshindwa kurejesha amani na usalama kwa wananchi wanaoteseka. Pia vikosi hivyo vimelaumiwa kushindwa kuzuia mashambulizi ya kidini nchini humo.

Mapigano hayo ya kidini yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 1,000 ndani ya mwezi Januari na kulazimisha watu zaidi ya milioni moja kuyakimbia makazi yao na mashamba yao.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment