ZITTO: MBUNGE ANAELILIA POSHO HASTAHILI...AKATAFUTE KAZI NYINGINE





Mwaka 2009 nikiwa mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya POAC nilikuta utamaduni wa Mashirika ya Umma/Taasisi za Serikali kuwalipa wabunge wanapoitwa kwenye kamati. Niliwashitaki Wabunge PCCB kwa matumizi mabaya ya madaraka na kujilipa posho ambazo hawastahili maana Bunge linakuwa limelipa. PCCB wakazuiwa uchunguzi wao na Spika Sitta, hata hivyo utamaduni huo ulikufa na siku hizi hakuna kitu kinachoitwa 'Parliamentary Expenses' kwenye mahesabu ya mashirika yote ya Umma.

PAC ilipiga marufuku Taasisi za Serikali au Mashirika ya Umma kulipa wabunge kwa kazi za kibunge. Hivyo hakuna hata mjumbe mmoja wa PAC anayelipwa posho na Taasisi yeyote ya Serikali kwa kazi za kibunge. Wajumbe wa PAC wanalipwa posho kama kamati nyingine, na posho za vikao mimi sichukui maana nimezikataa bungeni, nimezikataa Halmashauri ya Wilaya Kigoma, nimezikataa Baraza la Ushauri la Mkoa wa Kigoma. Hata nikialikwa na NGOs kwa kazi zangu za ubunge sichukui posho yeyote. It is a matter of principle!


Sipendi hata kidogo kulumbana na wabunge wenzangu kuhusu suala hili. Ni jambo la hiari ya mtu kuchukua au kutochukua posho. Hebu tujielekeze kutatua kero za wananchi badala ya kulumbana kunakosababisha tutunge uongo ili tu kulilia posho. Mbunge anayelilia posho hastahili kuwa mbunge. Akatafute kazi nyingine....
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment