WATANZANIA MBARONI NCHINI INDIA KWA KUBEBA MADAWA YA KULEVYA

 


Mtandao wa India today umechapisha habari kuwa Polisi mjini Mumbai inawashikilia Watanzania wawili waliokamatwa na madawa ya kulevya baada ya mwenzao wa tatu kufariki dunia.

Taarifa zinasema kuwa, baada ya polisi na kikosi maalumu cha kudhibiti madawa ya kulevya kutonywa, waliwakamata katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Chatrapati Shivaji mjini Mumbai.

Miongoni mwa Watanzania hao, wawili walikuwa wamebeba madawa ya kulevya na walikuwa wakisafiri kwa ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia. Baada ya kuhojiwa kwa muda wa saa 5, bado hawakukiri kubeba madawa. Ndipo walipopewa chakula na maji ili kujiridhisha.

Wabeba madawa huwa wanakataa kula au kunywa kwa sababu ya kuhofia madawa kupasukia tumboni na kusababisha kifo. Mmoja kati yao alikubali kula.

Baadaye watatu hao walipelekwa mahakamani, lakini yule aliyekubali kula chakula aligoma na kujaribu kutoroka. Ghafla alianguka nje ya mahakama na kufa katika hali iliyoonekana kuwa ni kuzidiwa na madawa. Inasemekana marehemu alikuwa amebeba kete 20 mpaka 25 za madawa.

Hali ya mtu wa pili ilizidi kuwa mbaya na alipelekwa hospitali ya JJ Jumatatu usiku. Baada ya vipimo vya X-ray na CT-scan, ilibainika kuwa alikuwa amebeba kete 100 tumboni.

Mtu wa tatu ni mwanamke wa makamu. Inaelezwa kuwa anahojiwa tofauti na wengine. Yeye hakubeba madawa, ila alikuwa pamoja nao, akiwasindikiza hao wengine, ambao ni wanaume.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment