AJALI YA TRENI YASABABISHA MAAFA NCHINI MISRI


ARCHIVE PHOTO: People inspect the wreckage of a train in Giza in Badrashin, located about 40 km south of Cairo, on January 15, 2013 (AFP Photo / Khaled Desouki)

KWA uchache watu 24 wamepoteza maisha na wengine 28 kujeruhiwa baada ya treni ya mizigo kuligonga basi dogo pamoja na gari ndogo la mizigo kusini mwa mji mkuu wa Misri, Cairo.

Kwa mujibu wa televisheni ya taifa pamoja na polisi, treni hiyo ilikuwa ilikuwa ikitokea katika mji wa Bani Swaif na kuyagonga magari katika wilaya ya Giza, kilometa 40 (maili 25) kutoka mji wa Cairo.

Majeruhi wengi ni ndugu wa familia moja waliokuwa wakisafiri katika basi wakitokea harusini.

Treni hiyo ilikuwa imebeba vifaa vya ujenzi, na wizara ya mambo ya ndani ya nchi hiyo imesema kuwa inachunguza chanzo hasa cha ajali hiyo.

Mkuu wa mamlaka ya usafiri wa reli nchini humo, Hussein Zakariya, ameliambia shirika la habari la nchi hiyo, MENA, kuwa magari hayo yalikuwa yakijaribu kuvuka eneo la reli ndipo yalipokutwa na zahma hiyo.


Usafiri wa reli nchini Misri unaelezwa kuwa na usalama mdogo ambapo mwaka 2012 wizara ya uchukuzi ya nchi hiyo ilikosolewa vikali baada watu 50, wengi wakiwa watoto, walipofariki dunia baada ya treni kuligonga basi la shule mjini Cairo.


Ajali mbaya kabisa kutokea nchini humo iliua watu 360 mwaka 2002, baada ya mabehewa yaliyokuwa yamebeba abiria kuwaka moto.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment