WALICHOSEMA MTEI NA BAREGU KUHUSU SAKATA LA ZITTO NA WENZAKE





MUASISI wa Chadema, Edwin Mtei ameelezea kusikitishwa na yaliyomkuta Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe, akisema kama kweli amekutwa na hatia ya kusaliti chama chake, basi haikuwa akili yake, bali ‘alirubuniwa’.

Alisema anavyomfahamu yeye, Zitto ni kijana makini na mwenye kujitambua.
Aidha, amesema kwa kuwa hakuhudhuria vikao vilivyobariki kuvuliwa madaraka kwa Zitto, Dkt Kitila na Samson Mwigamba, kwa sasa hawezi kuzungumza zaidi.

Alisema hayo jana kwa njia ya simu baada ya kutakiwa kuzungumzia uamuzi wa chama alichokiasisi wa kuwavua madaraka viongozi hao wenye nguvu na ushawishi kisiasa.
“Nasubiri nisikie wanazungumzaje kuhusu kuvuliwa kwao madaraka, baada ya kutafakari nitakuwa na kitu cha kuzungumza, kama kutakuwa na ulazima wa kufanya hivyo,” alisema.

BAREGU BADO YUPO

Kuhusu Uvumi wa mjumbe wa kamati Kuu ya Chadema, Profesa Mwesiga Baregu kujiuzulu kama ilivyokuwa kwa Makamu Mwenyekiti, Said Arfi, msomi huyo alisema hajafikiria kufanya hivyo.

Bali alikisihi chama hicho kuwaeleza kwa kina na ukamilifu wanachama wake kwa nini kimefikia uamuzi wa kuwavua madaraka Zitto na wenzake, badala ya kuwa na uamuzi mwingine.

Akizungumza kwa simu jana, Baregu alisema jambo muhimi ni kwamba, Zitto na wenzake hawajafukuzwa uanachama, hivyo wana nafasi ya kufanya mazungumzo ya maridhiano hususan katika mikutano mikubwa ya Baraza Kuu au Mkutano Mkuu ambayo ina nafasi ya kukubali au kukataa uamuzi huo.

Aliwataka wanachama kuwa watulivu kwa sasa na kuelewa sababu ya uamuzi huo na kutafakari ili wafanye uamuzi bila jazba au upendeleo.

Alisema kila chama kina katiba, taratibu na kanuni katika utendaji kazi, hivyo Kamati Kuu ilikuwa na haki ya kufanya uamuzi huo, lakini ni ushauri kwa vikao vya juu vilivyobaki.



Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment