HATIMAYE IRAN NA MATAIFA MAKUBWA WAFIKIA MAKUBALIANO

 إيران والقوى الكبرى تتوصل لاتفاق حول النووي



Na Kabuga Kanyegeri, Istanbul


IRAN na mataifa sita yenye nguvu zimefikia makubaliano kuhusu programu yake ya nishati ya nyuklia.

Akizungumza baada ya mazungumzo yaliyodumu kwa siku kadhaa mjini Geneva, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Mohammad Javad Zarif, amethibitisha kuwa   hatimaye Iran na mataifa hayo wamefikia makubaliano.

Naye Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa Laurent Fabius na msemaji wa mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya Catherine Ashton, Michael Mann, wametangaza kufikiwa kwa makubaliano hayo.

Makubaliano hayo yametangazwa leo baada ya mazungumzo mazito baina ya Iran na mataifa ya Uingereza, China, Ufaransa, Urusi Marekani na Ujerumani, ambayo yalikuwa yamepangwa kumalizika Ijumaa lakini yakaingia siku ya tano.

Makubaliano hayo ya muda yanairuhusu Iran kuendelea na shughuli zake kwenye vinu vya Arak, Fordo, na Natanz.

Kwa mujibu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, makubaliano hayo pia yanabainisha kuwa hakuna vikwazo zaidi vitakavyowekwa dhidi ya Iran kwa sababu ya programu yake ya nishati ya nyuklia.

Aidha, katika makubaliano hayo, Iran itaweza kupokea dola bilioni 4.2 kama sehemu ya makubaliano hayo.

Mwakilishi mkuu wa Iran kwenye mazungumzo hayo, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje Seyyed Abbas Araqchi, amesema kuwa kwa mujibu wa makubaliano hayo, Iran itaendelea na programu yake ya urutubishaji wa madini ya urani.

Awali Araqchi alikuwa amesisitiza kuwa Tehran isingekubali mpango wowote usiotambua haki ya nchi yake ya urutubishaji wa urani.


Makubaliano hayo ya aina yake yamefikiwa katika awamu ya tatu ya mazungumzo baina ya Tehran na Mataifa makubwa tangu kuingia madaraki kwa uongozi mpya wa taifa hilo chini ya Rais Hassan Rouhani aliyeingia madarakani Agosti mwaka huu. 
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment