WAANDAMANAJI: TUTAZIKAMATA WIZARA

Anti-government protesters wave national flags during a demonstration in Bangkok, November 25, 2013.
Waandamanaji wanaoipinga serikali wakipeperusha bendera za taifa mjini Bangkok, Novemba 25, 2013




WAANDAMANAJI wanaoipinga serikali nchini Thailand wametishia kuwa watazikamata wizara zote baada ya kuingia kwa nguvu katika majengo ya wizara ya fedha.

Waandamanaji hao waliokuwa na hasira waliingia kwa nguvu katika majengo ya wizara ya fedha na kulizingira eneo hilo wakimlazimisha Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Yingluck Shinawatra, ajiuzulu.

Waaandamanaji wanadai kuwa utawala wa Yingluck unadhibitiwa na kaka mkubwa wa Waziri Mkuu huyo, Thaksin Shinawatra, aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa nchi hiyo na kuondolewa na jeshi.

“Kesho tutazikamata wizara zote ili kuuonesha ukoo wa Thaksin kwamba hawana hati miliki ya kuongoza nchi hii,” alisema kiongozi wa upinzani, Suthep Thaugsuban, akiwahutubia waandamanaji mjini Bangkok.

Maandamano hayo yamechochewa na hatua ya serikali kupeleka muswada bungeni ambao utatoa msamaha kwa aliyekuwa Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Thaksin Shinawatra, ambaye anatuhumiwa kwa ufisadi na kutomheshimu mfalme anayetambuliwa na katiba ya nchi hiyo, Mfalme Bhumibol Adulyadej.

Thaksin Shinawatra aliondolewa madarakani mwaka 2006 katika mapinduzi ya jeshi kufuatia ugombaniaji wa madaraka baina ya wafuasi wake na wapinzania wake.


Waziri Mkuu huyo wa zamani amekuwa akiishi uhamishoni kwa miaka mitano sasa kwa hofu ya kushitakiwa na kutumikia kifungo gerezani kwa makosa ya ufisadi na ubadhirifu wa mali ya umma.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment