VOLKANO YAIBUA KISIWA KIPYA KATIKA BAHARI YA JAPAN



MLIPUKO wa volkano umeibua kisiwa kidogo jirani na pwani ya Japan. Walinzi wa Pwani ya Japan wametoa tahadhari baada ya kisiwa hicho kipya kutemea mvuke, moshi mweusi, majivu na mawe.

Kisiwa hicho kipya ni sehemu ya visiwa vingine vinavyojulikana kama Visiwa vya Bonin katika eneo la Ogasawara. Bonin ni kundi la visiwa 20 ambavyo havina wakazi na vipo kilometa 1,000 kutoka mji mkuu wa Japan. Kisiwa hicho kipya kinakadiriwa kuwa na mita 200 kwa kipimo cha diameter.

Wataalamu wanasema kuwa huwenda kisiwa hicho kikatoweka haraka au kikaendelea kuwepo na kuwa sehemu ya visiwa hivyo vingine.


Smoke from an erupting undersea volcano forms a new island off the coast of Nishinoshima, a small uninhabited island, in the southern Ogasawara chain of islands in this November 21, 2013 (Reuters / Kyodo)
Moshi wa volkano kutoka chini ya bahari iliyotengeneza kisiwa kipya kwenye pwani ya Nishinoshima, nchini Japan leo.




Tukio hilo lililotokea leo ni la kwanza katika eneo hilo tangu miaka ya 1970. Harakati nyingi za volkano katika hilo huwa hayabainiki au kuonekana kwa ababu mengi huishia ndani ya kina kirefu cha bahari.

Serikali ya Japan inaonekana kuwa makini sana na umiliki wa maeneo kwa sababu tayari ina imekuwa katika migogoro kadhaa ya mipaka na majirani zake. Hata hivyo, imelipokea tukio hilo na kulifurahia.


"Iwapo kitakuwa kisiwa kamili, tutafurahi kwa sababu tutakuwa tumeongeza eneo la nchi yetu," alisema msemaji wa serikali, Yoshihide Suga.


Smoke from an erupting undersea volcano forms a new island off the coast of Nishinoshima (top L), a small uninhabited island, in the southern Ogasawara chain of islands in this November 20, 2013 (Reuters / Japan Coast Guard / Handout via Reuters)
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment