MCHEZA SOKA WA KIKE WA TUNISIA ABADILI JINSIA NA KUITWA MOHAMMAD ALI

Fatima Maleh alifanyiwa vipimo na kupata cheti kilichoonesha kuwa ana homni za kiume.




Na Kabuga Kanyegeri

MCHEZA soka wa kike nchini Tunisia, Fatima Maleh, ametangaza kwenye radio moja ya kitaifa kuwa yeye ni mwanaume, ambaye ameandikishwa rasmi katika taarifa za kiraia kama  Mohammad Ali.

Maleh mwenye umri wa miaka 29 alipozaliwa aliandikishwa kama mtoto wa kike, ambapo familia yake, marafiki zake na wanafunzi wenzanke walimchukulia hivyo kwa miaka mingi.

“Nilipokuwa mtoto kila kitu kilikuwa sawa sawa, lakini mambo yalianza kubadilika nilipofikia umri wa baleghe,” Maleh alikiambia kituo cha habari za michezo,  Radio Nationale.

“Nilipovuka umri wa miaka 12 na 13 hakuna kilichotokea, nikaanza kujiuliza maswali, lakini sikupata majibu,” aliongeza kusema.

“Lakini nilianza kuhisi kuwa mimi sio mwanamke umri wangu ulipoongezeka kidogo na kuanza kuhisi kuvutiwa na mabinti,” alisema Maleh.

Alipokuwa sekondari, alianza kupenda kama watoto wa kiume. Alipenda kukaa na wavulana na kucheza nao soka, anasema.


Katika mji wake wa nyumbani wa Tataouine, unaopatikana kusini mwa Tunisia, haikuwa rahisi kwake kuandamana na wavulana. “Katika mji wa Tataouine sikuweza kucheza na wavulana; walikuwa wakinipiga kila ninapokwenda kucheza nao,” anasema.

Maleh alianza kuwa mchezaji wa kimataifa akichezea katika klabu moja katika nchi moja ya Ghuba.

Aliwaficha wachezaji wa klabu yake ya wanawake na kwamba hakuwa akijisikia  raha anapokuwa katika chumba cha kubadilishia nguo.

Baada ya miaka mingi ya usumbufu wa kisaikolojia kuhusu suala la kutaka kubadilisha jinsia, hatimaye alianza mchangato wa kubadilisha jinsia yake kwa taratibu za kiserikali kabla ya kuiweka hadharani siri yake.

Hatua ya kuingia katika mahusiano na mkewe mtarajiwa ilimfanya azidi kuliweka hadharani suala hilo.

Mwaka 2008 alifanyiwa vipimo na kupata cheti kinachomuonesha kuwa alikuwa na homoni nyingi za kiume na sifa za misuli ya mwili wake kuwa ni ya kiume.

“Via vyangu vya uzazi vinaonekana zaidi kuwa kama vya mwanaume,” alisema.

Kutokana na ceti hicho, Maleh aliweza kupata idhini ya mahakama ya kubadilisha rikodi za jinsia yake katika kitambulisho chake za taifa pamoja na nyaraka nyingine.


Anasema kuwa  Juni 24, 2013 alifanikiwa kupokea kitambulisho chake kipya kikiwa na jina lake alilochagua la Mohammad Ali.

CHANZO: Al-Arabiya
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment