NAIBU MKUU WA SHIRIKA LA UJASUSI LIBYA ATEKWA NYARA


Naibu Mkuu wa shirika la ujasusi Libya atekwa nyara

Naibu wa Mkuu wa Shirika la Kijasusi la Libya ametekwa nyara akiwa pamoja na mmoja wa viongozi waliooongoza mapinduzi dhidi ya Kanali Muammar Gadafi nchini humo. Televisheni ya al Jazeera ya Qatar imeripoti kuwa, maafisa hao waandamizi wa Libya wametekwa nyara leo mjini Tripoli. Huku hayo yakiripotiwa, habari kutoka Tripoli, mji mkuu wa Libya zinasema kuwa, hali ya wasiwasi imerejea mjini humo baada ya kutulia kwa muda mfupi.

Kwa siku mbili mfululizo mji huo umeshuhudia mapigano kati ya pande hasimu yaliyopelekea zaidi ya watu 40 kuuawa na karibu laki tano wengine kujeruhiwa. Leo wananchi wa Libya wameendelea kuwazika watu waliouawa, maziko ambayo yameambatana na maandamano ambapo wakazi wa mji huo wameitaka serikali dhaifu ya nchi hiyo ikabiliane vilivyo na wanamgambo wenye silaha.


Wananchi hao wametishia kufanya uasi wa nchi nzima kama serikali na makundi yenye silaha yatashindwa kufikia makubaliano ya kurejesha amani katika nchi hiyo tajiri kwa mafuta ya kaskazini mwa Afrika.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment