MAFURIKO YALETA BALAA VIETNAM

 A scene of flood water caused by a tropical depression in central Vietnam on November 15, 2013

Na Kabuga Kanyegeri

WATU thelathini na nne wamepoteza maisha na wengine kadhaa kupotea baada ya jimbo la kati nchini Vietnam kukumbwa na mafuriko makubwa kuwahi kutokea kwa zaidi ya muongo mmoja.

Mvua kubwa iliyotokana na mgandamizo wa kimbunga Haiyan kilichopiga katika Bahari ya Kusini mwa China kimesababisha mafuriko ambayo hayajawahi kutokea tangu mwaka 1999.

Mafuriko yaliyodumu kwa siku kadhaa yamezigharikisha nyumba na barabara katika mji wa Hoi An na jiji la Hue, na kuwalazimisha watu wapatao 80,000 kuuhama mkoa huo.

Zaidi ya nyumba 100,000 zimegharikishwa huku usafiri wa barabara, anga na reli ukiathiriwa vibaya sana katika jimbo hilo na mvua imeendelea kunyesha katika wilaya za pwani za Quang Ngai na Binh Dinh – ambapo watu wapatao 20 (kati ya 34) wamepoteza maisha.
Hasara iliyotokana na mafuriko hayo inakadiriwa kufikia dola za kimarekani milioni 65.

Maelfu ya watu walihamishwa kabla ya kufika kwa Kimbunga Haiyan, ambacho kiliiathiri vibaya sana nchi ya Ufilipino, kabla ya kuelekea Katika Bahari ya Kusini mwa China.

Mamlaka nchini Ufilipino na Umoja wa Mataifa zimetoa idadi ya vifo inayotofautiana, vinavyokadiriwa kufukia zaidi ya watu 3,600. Idadi ya makadirio ya majeruhi ni 12,487, huku watu 1,187 wakiripotiwa rasmi kuwa wamepotea.


Matukio hayo mapya yanakuja baada ya mvua za msimu zilizosababishwa na Kimbunga Usagi kuyapiga maeneo kadhaa ya nchi za Vietnam na Cambodia mapema mwezi jana na kugharimu maisha ya watu 40.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment