AJALI YA NDEGE YAUA 52 URUSI


Boeing 737


WATU wasiopungua 52 wamepoteza maisha baada ya ndege aina ya Boeing 737 kuanguka nchini Urusi.

Kwa mujibu wa msemaji wa Wizara ya Majanga na masuala ya dharura, Irina Rossius, ndege hiyo inayomilikiwa na shirika la ndege la Tatarstan Airlines ilipata ajali hiyo katika mji wa Kazan, katikati mwa Urusi na kuua watu wote waliokuwemo, ambao ni wafanyakazi 6 na abiria 46.

Mamlaka zinasema kuwa ndege hiyo ilijaribu kutua mara mbili lakini ikashindwa na kuanguka katika jaribio la tatu.

Ndege hiyo iliyokuwa imetoka katika uwanja wa ndege wa Domodedovo, ilishika moto baada ya kuanguka katika mji wa Kazan, karibu kilometa 720 mashariki mwa mji mkuu wa Urusi, Moscow.  


Hakujatolewa dalili zozote zinazoweza kuwa chanzo cha ajali ya ndege hiyo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment