MAMIA WAUAWA KATIKA MAPIGANO YA KIKABILA NCHINI SUDAN

The file photo shows a camp for internally displaced people in Nyala, the capital of South Darfur.
Kambi ya wakimbizi wa ndani katika mji mkuu wa Jimbo la Darfur, Nyala



Na Kabuga Kanyegeri

WATU wapatao mia moja, wakiwemo askari wa Chad, wameuawa katika mapigano ya kikabila katika jimbo la Darfur, magharibi mwa Sudan.

Radio Omdurman ya nchini humo imeripoti kuwa vifo hivyo vilitokana na mapigano baina ya makabila ya Misseriya na Salamat, ambayo yamekuwa na uadui na uhasama kwa miaka mingi, na mwezi huu uhasama umeibua mapigano makali baina yao.


Kwa mujibu wa kiongozi wa kabila la Misseriya, mapigano kati ya makundi hayo uliendelea jana karibu na eneo la Umm Dukhun, karibu na mpaka wa nchi hiyo na nchi ya Chad na kugharimu maisha ya watu 50 kutoka pande mbili.

Aidha, siku hiyo hiyo, chanzo kimoja kilieleza kuwa askari kadhaa wa Chad waliuawa katika mapigano na kabila la Salamat karibu na eneo la Umm Dukhun yaliyotokea siku ya Alhamisi.



Ripoti zinasema kuwa tangu Aprili mwaka huu watu wapatao 200 wameshapoteza maisha yao katika mapigano baina ya makabila hayo mawili.

Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoratibu misaada ya kibinadamu (OCHA) inasema kuwa mwaka huu migogoro ya kikabila na uasi vimesababisha watu wapatao 460,000 kuyahama makazi yao katika jimbo la Darfur.

Mnamo Novemba 13, Waziri wa Ulinzi wa Sudan, Abdulrahim Mohammed Hussein alisema kuwa ghasia za kikabila katika jimbo la Darfur zimekuwa hatari kwa usalama wa eneo hilo kuliko hata mapigano ya waasi.

Tarehe 12 Novemba, misheni ya Umoja wa Mataifa katika jimbo la Darfur, UNAMID, ilielezea “wasiwasi mkubwa” kutokana na ripoti za ghasia za hivi karibuni baina ya makabila ya Misseriya, Taisha, na Salamat katika eneo la katikati mwa jimbo la Darfur.

Sudan inaituhumu Sudan Kusini, ilijitoa kutoka Jamhuri ya Sudan Julai 2011, kuwa inayasaidia makundi yanayoipinga serikali yanayopatikana Darfur na katika majimbo ya Blue Nile na Kordofan Kusini.


Sudan Kusini ilipata uhuru wake Julai 9, 2011, baada ya miongo kadhaa ya mapigano baina yake na Sudan Kaskazini.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment