WATU 10 WAPOTEZA MAISHA KATIKA AJALI YA TRENI NCHINI KENYA

 

WATU kumi wamethibitika kupoteza maisha kufuatia ajali iliyoihusisha treni na daladala katika eneo la Umoja mjini Nairobi, Kenya.

Mkuu wa kikosi cha reli, Kirimi Ringera amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa, miongoni mwa waliopoteza maisha ni wanaume watano na wanawake watano, huku wengine 21 wakiwa wamejeruhiwa vibaya sana na kupelekwa hospitalini.

Ajali hiyo ilitokea wakati daladala ikijaribu kuvuka reli ndipo treni ilipoigonga.

Kwa mujuibu wa mashuhuda, daladala hiyo ilisukumwa umbali wa mita 500 kutoka kwenye eneo la ajali.

CHANZO: KTN Kenya


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment